SOMA:-Onyo la Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA )kwa Itv na Star tv pamoja na Radio Free,kutokana na kurusha Tangazo ambalo linakwenda kinyume na Maadili. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, March 07, 2014

SOMA:-Onyo la Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA )kwa Itv na Star tv pamoja na Radio Free,kutokana na kurusha Tangazo ambalo linakwenda kinyume na Maadili.


Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakiwa wanasikiliza kwa umakini mkutano wa wa kamati ya maudhui kutoka Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) leo March 07,2014,wakati wa uwasilishaji maamuzi ya kamati hiyo juu ya vituo vya Itv na Startv pamoja na RadioFree,kutokana na kurusha.


Mkurugenzi wa Itv na Radio One,Bi Joyce Mhavile akiwa katika mkutano huo ambao umefanyika katika ukumbi wa Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) jijini dar es Salaama juu ya kuvipa onyo kali vyombo hivyo.

Mwenyekiti wa kamati ya maudhui kutoka Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA)akiwasilisha maamuzi ya kamati hiyo juu ya vituo hivyo vya kurusha matangazo ,mbele ya waandishi wa habari leo March 07,2014.

Na:- Karoli Vinsent

Mamlaka ya Mawasiliano nchini Tanzania (TCRA) imevipa onyo kali televisheni ya Itv na Startv pamoja na RadioFree,kutokana na kurusha Tangazo ambalo linakwenda kinyume na Maadili.

Hayo,yalisemwa leo March 07,2014,Jijini Dar es Salaam katika  mkutano na Waandishi wa Habari  na Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka hiyo,Margaret Mnyagi ambapo alisema Kamati imefikia maamuzi hayo baada ya kushauriana na Kamati Maudhui ya vipindi vya Runinga vya mamlaka hiyo.

Tumefika maamuzi haya baada ya kukaa sisi kama kamati ya Maudhui na kubaini tangazo la Policy Forum ambalo tangazo hilo linachochoe watu wasilipekodi,Tangazo hilo lilirushwa kwenye Runinga mbili ambazo ni Itv pamoja na Startv na redio ambayo ni Radio Free”

Napenda kuwatoa hofu wananchi kuwa atuchafanya upendeleo wowote katika kutoa hukumu hii”alisema Mnyagi

Aidha Mamlaka hiyo imevitaka vyombo hivyo vilivyorusha Tangazo hilo viwasilishe mwongozo wa urushaji wa Matangazo hayo,na  pia Mamlaka hiyo imevionya vyombo hivyo kutorudia kuonyesha Matangazo ya Uchochezi na endapo watakaidfi Mamlaka hiyo itawachukulia hatua kali za kisheria.
  
Kwa upande wake Meneja wa Mipango na Utafiti wa Sahara Media  Bw. Nassani Lwehabula ambao  ni wamiliki wa Star tv,Kiss fm,Radio free,Gazeti la Msanii wa Afrika alisema wao wamechukulia Hukumu hiyo ni kama Changamoto kwao ya kufanya Vipindi vyao kuwa na umakini ili waweze kukuza maudhui yao,

Ikumbukwe Tangazo liloifanya Mamlaka ya Mawasiliano nchini kuchukua Maamuzi hayo ni Tangazo la Taasisi isiyokuwa ya kiSerikali inayojulika PolcyForum,ambapo katika Tangazo hilo linawahamasisha wananchi wasilipe kodi mwenzi Januari Mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad