Picha ya Ajali ikiua mtu mmoja baada ya Lori la mafuta lililogongana na basi dogo eneo la Bwawani mkoani Pwani. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, March 07, 2014

Picha ya Ajali ikiua mtu mmoja baada ya Lori la mafuta lililogongana na basi dogo eneo la Bwawani mkoani Pwani.


Dereva wa lori la mafuta, Ally Hassan Ngoma (62) mkazi wa Korogwe amefariki dunia papo hapo baada ya kutokea ajali iliyohusisha gari tatu ikiwemo basi ndogo, lori na basi kubwa kugongana uso kwa uso na kusababisha kifo cha mtu mmoja na majeruhi 38 katika ajali iliyotokea eneo la Bwawani majira ya saa 4:30 asubuhi jana March 06,2014,mkoani Pwani.


Muonekano wa basi hilo aina ya Toyota Coaster lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Ifakara likionekana kuharibika kwa ndani baada ya kugongana na lori la mafuta lililokuwa likitoka Morogoro kuelekea Chalinze.

Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Chalinze mkoani Pwani, Innocent Sull akiangalia lori la mafuta lililogongana na basi dogo eneo la Bwawani na kusababisha kifo cha mtu mmoja.

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine 14 kujeruhiwa baada ya basi dogo kugongana uso kwa uso na lori katika eneo la Bwawani katika Barabara ya Chalinze - Morogoro. 
 
Ajali hiyo ilitokea jana (March 06,2014) saa 4.30 asubuhi baada ya basi hilo aina ya Toyota Coaster lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Ifakara kugongana na lori la mafuta lililokuwa likitoka Morogoro kuelekea Chalinze.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Ulrich Matei alimtaja aliyefariki dunia katika ajali hiyo ni dereva wa lori, Ally Ngoma (62).
 
Kamanda Matei alisema majeruhi 14 wa ajali hiyo ni abiria waliokuwa kwenye basi. Alisema wote walipelekwa katika Kituo cha Afya Chalinze kwa matibabu.
 
Alisema ajali hiyo ilitokea baada ya dereva wa basi kujaribu kuyapita magari mengine katika eneo la Sekondari ya Bwawani sehemu ambayo ina mwinuko.
 
Alisema wakati dereva huyo akijaribu kuyapita magari hayo, alikutana na lori hilo na kugongana uso kwa uso na kusababisha kifo na majeruhi hao.
 
Alisema dereva wa basi hilo anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote kuanzia sasa kujibu tuhuma zinazomkabili.
 
Mbali ya kusababisha kifo na majeruhi hao, ajali hiyo ilisababisha adha kwa waliokuwa wakitumia barabara hiyo hasa wale wanaosafiri kati ya Dar es Salaam na Morogoro kwani zaidi ya magari 200 yalikwama kwa zaidi ya saa tatu.
 
Ajali hiyo imetokea siku moja baada ya nyingine iliyosababisha vifo vya watu saba baada ya basi dogo la abiria kugongana na lori katika eneo la Chalinze Mzee na kujeruhi tisa.
 
Akizungumzia ajali hiyo ya juzi, Ofisa Habari wa Hospitali ya Tumbi, Kibaha, Gerald Chami alisema majeruhi sita hali yao wanaendelea vyema.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad