Mkuu wa
wilaya ya Ngara, Bw Constantine Kanyasu amebainisha hayao March 20,2014, wakati
akisoma taarifa ya wilaya hiyo ,kwa mkuu
wa mkoa wa Kagera Kanal Mstaafu Fabian Masawe aliyefanya ziara ya kutembelea
miradi ya maji wilayani humo ikiwa ni sehemu
ya maadhimisho ya Wiki ya Maji.
Bw Kanyasu
amesema kuwa Rais ametuma fedha hizo ili
kuboresha na kupanua mradi wa maji mjini Ngara na kwamba fedha hizo zitatumika kwa kununua mtambo mpya
wa kusukuma maji utakaofungwa katika kisima kipya kilichochimbwa pamoja na
kuongeza vyanzo vya maji kutoka visima viwili virefu hadi kufika visima vitatu .
Bw Kanyasu amewataka
wataalam katika Mamlaka ya Maji na viongozi wengine kuhakikisha fedha hizo
zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuondokana na malalamiko ya wananchi kuhusu
huduma ya maji isiyokidhi mahitaji na Kuongeza uzalishaji wa maji kutoka
kiwango cha sasa cha 76%.





No comments:
Post a Comment