Ligi Kuu
Vodacom, iliendelea Leo March 08,2014 na huko Uwanja wa Sokoine, Jijini Mbeya, Wana wa
Nyumbani, Mbeya City, wameicharaza Rhino Rangers ya Tabora Bao 3-1 na kukamata
Nafasi ya Pili na kuwashusha Mabingwa Watetezi Yanga toka Nafasi hiyo.
Mbeya City
sasa wamecheza Mechi 21 na wana Pointi 39 wakiwa Pointi 1 moja mbele ya Yanga
SC, ambao wamecheza Mechi 17 tu, na Pointi 1 nyuma ya Vinara Azam FC waliocheza
Mechi 18.
Huko
Mkwakwani, Tanga, Wenyeji Coastal Union walitoka 0-0 na Ashanti United na huko
Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Mkoani Pwani, Ruvu Shooting iliitungua JKT Oljoro
Bao 1-0 kwa Bao la Ayub Kitala.
Ligi
itaendelea Jumapili kwa Mechi mbili huko Mbeya na Dar es Salaam ambako Uwanja
wa Sokoine, Mbeya, utakuwa na Mechi ya Tanzani Prisons na Simba SC na huko Azam
Complex, Chamazi, Viunga vya Dar es Salaam, JKT Ruvu watacheza na Mtibwa Sugar.
LIGI KUU
VODACOM TANZANIA BARA 2013/2014.
Jumapili
Machi 9,2014.
Tanzania
Prisons v Simba
JKT Ruvu v
Mtibwa Sugar
MATOKEO.
Jumamosi
Machi 8,2014.
Coastal
Union 0 Ashanti United 0
Mbeya City 3
Rhino Rangers 1
Ruvu
Shooting 1 JKT Oljoro 0
MSIMAMO.
| NA | TIMU | P | W | D | L | GD | PTS |
| 1 | Azam FC | 18 | 11 | 7 | 0 | 23 | 40 |
| 2 | Mbeya City | 21 | 10 | 9 | 2 | 10 | 39 |
| 3 | Yanga SC | 17 | 11 | 5 | 1 | 29 | 38 |
| 4 | Simba SC | 20 | 9 | 8 | 3 | 17 | 35 |
| 5 | Kagera Sugar | 20 | 7 | 8 | 5 | 2 | 29 |
| 6 | Ruvu Shooting | 20 | 7 | 7 | 6 | -4 | 28 |
| 7 | Coastal Union | 20 | 5 | 11 | 4 | 5 | 26 |
| 8 | Mtibwa Sugar | 19 | 6 | 7 | 6 | 0 | 25 |
| 9 | JKT Ruvu | 20 | 7 | 1 | 12 | -14 | 22 |
| 10 | Prisons FC | 18 | 3 | 9 | 6 | -3 | 18 |
| 11 | Mgambo JKT | 20 | 4 | 6 | 10 | -17 | 18 |
| 12 | Ashanti United | 21 | 4 | 6 | 11 | -18 | 18 |
| 13 | JKT Oljoro | 21 | 2 | 9 | 10 | -16 | 15 |
| 14 | Rhino Rangers | 21 | 2 | 7 | 12 | -14 | 13 |






No comments:
Post a Comment