![]() |
|
Mto Ruvubu/Ruvuvu ukionekana ambapo hukutana na maji ya Mto Kagera na kutengeneza maporomoko ya Rusumo.
|
![]() |
|
Maporomoko ya Rusumo yakipatikana wilayani Ngara mkoani Kagera mpakani mwa Tanzania na
Rwanda-Daraja la rusumo).
|
Mkuu wa Mkoa
wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massawe ameiagiza Mamlaka ya maji safi na usafi
wa mazingira wilayani Ngara mkoani humo, kuanza kuzikatia huduma ya maji
taasisi za serikali zinazodaiwa zaidi ya Sh milioni 8 na laki 3.
Kanali
Massawe ametoa agizo hilo leo March 20,2014, wilayani Ngara, muda mfupi baada
ya kusomewa taarifa ya wilaya hiyo, kuhusu maadhimisho ya wiki ya maji,
iliyosomwa na Mkuu wa wilaya ya Ngara Bw Constantine Kanyasu.
Amesema
serikali haitazivumilia taasisi zake zinazolimbikiza Ankara za maji, hali
inayosababisha kukwama kwa utoaji wa huduma ya maji kwa wananchi.
Akisoma
taarifa ya wilaya, Mkuu wa wilaya ya Ngara Bw Costantine Kanyasu amesema kuwa
taasisi za Magereza na Polisi, hadi kufikia mwezi Februari mwaka huu zilikuwa
zinadaiwa zaidi ya Sh milioni 8 na laki 3 hali inayosababisha kukwama kwa
shughuli za usambazaji maji.
Habari Na:-Radio
Kwizera FM.








No comments:
Post a Comment