BREAKING NEWS:- Mkuu wa Mkoa wa Mara aanguka ghafla na kufariki Dunia. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, March 25, 2014

BREAKING NEWS:- Mkuu wa Mkoa wa Mara aanguka ghafla na kufariki Dunia.


Mkuu wa mkoa Mara, Bw John Gabriel Tuppa, (enzi ya uhai wake)amefariki dunia ghafla leo March 25,2014,majira ya saa 4.30 asbuhi baada ya kuugua kwa muda mfupi ugonjwa wa shinikizo la damu akiwa wilaya ya Tarime mkoani Mara.


Katibu tawala wa mkoa wa Mara, Bw Benedict Ole Kuyan, amesema kuwa Bw. Tuppa kabla ya kifo chake leo asubuhi akiwa na afya njema alifika katika ofisi za mkoa na kumuaga kuwa anakwenda kufunga mafunzo ya mgambo katika kijiji cha Nyamwaga wilayani Tarime.

Amesema kuwa muda mfupi baada ya kufika katika ofisi ya mkuu wa wilaya, alipatwa na tatizo la ugonjwa huo na muda mfupi alikimbizwa hospitali ya Tarime lakini alifariki wakati akipatiwa matibabu.

Katibu tawala huyo amesema mwili wa marehemu unasafarishwa kutoka Tarime kuja hospitali ya Musoma kwa ajili ya kuhifadhiwa wakati taratibu nyingine na maelekezo ya kiserikali yakisubiriwa kutolewa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad