Yanga SC yawakung’uta 7-0 Wacomoro katika mchezo wa kwanza wa raundi ya Awali, Ligi ya Mabingwa Afrika. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, February 08, 2014

Yanga SC yawakung’uta 7-0 Wacomoro katika mchezo wa kwanza wa raundi ya Awali, Ligi ya Mabingwa Afrika.


Mabao hayo yalifungwa na Ngassa dakika ya 14 na Cannavaro dakika ya 20, wote wakitikisa nyavu kwa kichwa baada ya mipira kutoka pembeni.
Yanga SC imetanguliza mguu mmoja Raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika, kufuatia ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Komorozine ya Comoro jioni hii katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Awali, Ligi ya Mabingwa Afrika.

Washambuliaji Mrisho Khalfan Ngassa alifunga mabao matatu, Mrundi Didier Kavumbangu mawili, Mganda Hamisi Kiiza moja na lingine beki Nadir Haroub Ali ‘Cannavaro’.

Kwa ushindi huo, Yanga sasa inahitaji sare au kufungwa si zaidi ya mabao 6-0 katika mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo ugenini ili kusonga mbele, ambako itakutana na Al Ahly ya Misri.

Nayo Azam inaikaribisha Ferroviario de Beira ya Msumbiji katika mchezo wa kwanza wa raundi ya awali ya CC utakaochezwa Jumapili (Februari 9 mwaka huu) saa 10 kamili kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad