Tazama Taswira ya Ajali kati ya Lori aina ya Scania likigongana uso kwa uso na Basi dogo la Abiria na kusababisha Majeruhi eneo la Mwandege. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, February 24, 2014

Tazama Taswira ya Ajali kati ya Lori aina ya Scania likigongana uso kwa uso na Basi dogo la Abiria na kusababisha Majeruhi eneo la Mwandege.

Picha ni baadhi ya abiria wakiwa kwenye hali  ya taharuki baada ya lori scania namba T653 BFD  (scania 380) kugongana uso kwa uso na baso dogo la abiria Toyota Hiace T613 CPG iliyokuwa inatoka mbagala kwenda mkuranga jana februari 23,2014.

Picha juu ni baadhi ya abiria wakiwa kwenye hali taharuki  baada ya lori scania namba T653 BFD  (scania 380) kugongana uso kwa uso na baso dogo la abiria Toyota Hiace T613 CPG iliyokuwa inatoka mbagala kwenda mkuranga jana februari 23,2014.
Watu wanne wapo katika hali mbaya na wengine saba wamejeruhiwa baada ya lori scania namba T653 BFD  (scania 380) kugongana uso kwa uso na baso dogo la abiria Toyota Hiace T613 CPG iliyokuwa inatoka mbagala kwenda mkuranga.

Kwa mujibu wa shuhuda ya ajali hiyo iliyotokea Mwandege, Dominic Kubhota, ameiambia blogu hii , kwamba chanzo cha ajali hiyo ni ovateki isiyotumia akili ya lori hilo . 

Majeruhi hao wamefikishwa katika hospitali ya Mkuranga, lakini muda mfupi baadaye walianza kukimbizwa kuleta Dar es Salaam kwa matibabu zaidi.

Abiria wawili waloikuwa mbele  ya daladala walikatika miguu.

Majeruhi wengine walioweza kuzungumza ni: Mustafa Mfungapoa wa mkuranga, Abdul Ally wa Mwandege, Ramadhani Rajab, Theofrida Mwinuka ( alikuwa mbele amevunjika miguu)Jamal  mbaraka ( aliyekwanguka ngozi ya kichwa)Abraham Mohamed
Swalehe Salum.

Picha na Lukaza Blog.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad