Tazama Picha za ukumbi wa Bunge tayari kwa Bunge la Katiba linalotarajiwa kuanza tarehe 18 ,Februari 2014 mjini Dodoma. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, February 10, 2014

Tazama Picha za ukumbi wa Bunge tayari kwa Bunge la Katiba linalotarajiwa kuanza tarehe 18 ,Februari 2014 mjini Dodoma.

Spika wa Bunge Mhe. Anna Makinda akijaribu mojawapo ya viti vipya vilivyofungwa katika ukumbi wa Bunge tayari kwa ajiri ya Matumizi wakati wa Bunge la Katiba. Mhe. Makinda aliongoza ujumbe wa Tume ya Utumishi wa Bnge kufanya ukaguzi wa mwisho kabla ukumbi huo haujakabidhiwa kwa Sekretariat ya Bunge la Katiba Jumatano wiki hii.

Spika wa Bunge Mhe. Anna Makinda, (katikati) Naibu Spika Mhe. Job Ndugai (kushoto), Katibu wa Bunge (Wa pili Kulia) na Mhe. Hamadi Rashid Mohamed Kulia wakiangalia baadhi ya maboresho yaliyofanywa katika Ukumbi wa Bunge kwa ajili ya Bunge la Katiba.
Muonekano wa Ndani ya ukumbi huo baada ya kazi ya uwekaji viti kukamilika.
Mojawapo ya viti maalum vilivyowekwea katika ukumbi huo kwa ajili ya matumizi ya watu wenye ulemavu, kwa ajiri ya matumizi ya Bunge la Katiba.
Viti vyote vipya vina nembo ya taifa,ukumbi wa Bunge kwa ajiri ya matumizi ya Bunge la Katiba.
Spika wa Bunge Mhe. Anna Makinda pamoja na Wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Bunge wakiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi walioshiriki kuukarabati ukumbi wa Bunge kwa ajiri ya matumizi ya Bunge la Katiba. Picha kwa hisani ya Bunge.
Tayari Serikali ya Tanzania imetangaza majina ya wajumbe walioteuliwa kushiriki bunge la katiba linalotarajiwa kuanza tarehe 18 ya mwezi huu mjini Dodoma.

Majina hayo yametangazwa ijumaa Februari 07,2014 jioni na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi Florence Turuka mbele ya waandishi wa habari ikulu jijini Dar es salaam.

Wajumbe wa bunge ni Wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar na Wajumbe 201 walioorodheshwa kwa mujibu wa Kifungu Na. 22(1c) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ambayo inaonyesha makundi mbalimbali 10 yanayohusika.

Majina hayo yametangazwa siku moja toka Rais wa nchi hiyo Jakaya Mrisho kikwete kuwaonya watakaoteuliwa kusimamia maslahi ya Taifa na kuweka kando itikadi zao.

Akizungumza katika kikao cha Baraza la Vyama vya siasa siku ya alhamisi jijini Dar es salaam, Rais Kikwete alisema Watanzania wanatarajia kuona mchakato huo ukiendeshwa kwa amani na utulivu hivyo wajumbe wote na vyama vya siasa watangulize mbele maslahi ya Taifa badala ya kuweka mbele maslahi binafsi au ya vyama vyao.

Baadhi ya majina yaliyoingia ni Prof. Ibrahim Lipumba, prof. Abdalah Safari , Paul kimiti, Kingunge Ngombale Mwiru, Peter Kuga mziray, Christoper Mtikila, John Lifa Chipaka, Emmanuel Makaidi ,Godfrey Simbeye, Kajubi Mukajaga, Paul Makonda na Julius Itatiro.

Bunge la katiba litakutana kwa siku 70 na huenda likaongezewa siku 20 zaidi endapo hakutakuwa na maafikiano ili kujadili rasimu ya pili ya katiba iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka jana.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad