CHEKI MATOKEO YA LIGI ULAYA 2013/2014:- Man United wachapwa 2-1 Uwanjani Britannica huku FC Barcelona wakipigwa 3-2 Nou Camp na sasa Atletico Madrid au Real Madrid kuwapiku uongozi wa Ligi?. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, February 02, 2014

CHEKI MATOKEO YA LIGI ULAYA 2013/2014:- Man United wachapwa 2-1 Uwanjani Britannica huku FC Barcelona wakipigwa 3-2 Nou Camp na sasa Atletico Madrid au Real Madrid kuwapiku uongozi wa Ligi?.

Magoli mawili ya Charlie Adam yameipa Stoke City ushindi wa kwanza kabisa kihistoria dhidi ya Manchester United katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza uliochezwa Jumamosi Feb 01,2014 katika Uwanja wa Britannia…ambapo Adam alifunga mabao hayo dakika ya 38 na 52, wakati bao pekee la Man United lililofungwa dakika ya 47 na Robin van Persie.


Kiungo mpya wa United, Juan Mata alicheza kwa dakika zote 90 na hakuweza kuwaepusha Mashetani hao Wekundu na kipigo. United sasa inabaki na pointi 40 baada ya kucheza mechi 24 na inaporomoka hadi nafasi ya saba kutoka ya sita.

RVP: Robin van Persie (20) akishangilia na wenzake wa Man Utd baada ya kuifungia bao la kusawazisha dakika ya 47 ya mchezo.

Kocha wa Man Utd, David Moyes akiwa na machungu baada ya timu yake kupigwa huku wachezaji wake Jonny Evans na Phil Jones wakiumia ambapo Jones alikimbizwa hospitali.


Manchester United imeendelea kusuasua katika Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kupokea kichapo cha bao 2-1 kutoka kwa Stoke City  jana Jumamosi (Februari 01,2014)  ikiwa ni mechi ya nane kupokea vipigo katika ligi hiyo.

Ushindi huo wa Stoke City ni wa kwanza kwenye Ligi tangu Mwaka 1984 dhidi ya Man United Uwanjani Britannica.

Mabao yote ya Stoke yamefungwa na Charlie Adam katika dakika ya 38 na 52 wakati bao la Manchester United likifungwa na Robin van Persie dakika ya 47. Kwa matokeo ya leo, Man Utd imebaki na pointi zake 40.

Katika mechi ya leo, wachezaji wawili wa Man Utd, Jonny Evans na Phil Jones waliumia ambapo Jones alikimbizwa hospitali kwa matibabu zaidi baada ya kugongana na Jon Walters wa Stoke.


    Newcastle 0 - 3 Sunderland
    West Ham 2 - 0 Swansea
    Cardiff 2 - 1 Norwich
    Everton 2 - 1 Aston Villa
    Fulham 0 - 3 Southampton
    Hull 1 - 1 Tottenham
    Stoke 2 - 1 Man Utd     

Position Team Played Goal Difference Points
    
      LIGI KUU UINGEREZA  RATIBA MECHI ZIJAZO.

[Saa za Bongo]

Jumapili Februari 2,2014.

16:30 West Brom v Liverpool
 19:00 Arsenal v Crystal Palace

Jumatatu Februari 3,2014.

23:00 Man City v Chelsea

1 Man City 23 42 53
2 Arsenal 23 24 52
3 Chelsea 23 23 50
4 Liverpool 23 29 46
5 Everton 24 12 45
6 Tottenham 24 -1 44
7 Man Utd 24 10 40
8 Newcastle 24 1 37
9 Southampton 24 7 35
10 Aston Villa 24 -7 27
11 Stoke 24 -14 25
12 Swansea 24 -6 24
13 Hull 24 -7 24
14 Sunderland 24 -11 24
15 Norwich 24 -18 24
16 Crystal Palace 23 -16 23
17 West Brom 23 -6 22
18 West Ham 24 -9 22
19 Cardiff 24 -22 21
20 Fulham 24 -31 19

LIGI KUU SOKA HISPANIA :- LA LIGA.

 
Timu ya Valencia imefanikiwa kufanya kweli Uwanjani Nou Camp na kuichapa Barcelona Bao 3-2 na kuwaweka Mabingwa hao kwenye njia panda maana Jumapili (feb 02,2014) Atletico Madrid au Real Madrid zina nafasi kubwa kuwapiku uongozi wa Ligi.

FC Barcelona walitangulia kufunga Bao katika Dakika ya 7 Mfungaji akiwa Alexis Sanchez na Valencia kujibu na kupiga Bao mbili katika Dakika ya 44 lililofungwa na Parejo na Dakika 4 baadae kupitia Pablo Piatti.

Barca walisawazisha kwa Penati ya Lionel Messi na hilo ni Bao lake la kwanza baada kutofunga katika Mechi 3 lakini Paco Alcácer, katika Dakika ya 59, aliipigia Valencia Bao la 3 na kuwapa ushindi.

Barca walimaliza wakiwa Mtu 10 baada Jordi Alba kupewa Kadi ya Njano ya pili kwenye Dakika ya 78 na kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.

Ukiiondoa Real Madrid, Valencia imekuwa Timu ya kwanza kuondoka Nou Camp bila kufungwa tangu Oktoba 2011 Sevilla ilipopata Sare ya 0-0.

Matokeo haya yameiacha Barca uongozini ikiwa Pointi 54, sawa na Atletico Madrid, lakini Atletico wana Mechi moja mkononi ambayo watacheza Nyumbani kesho Jumapili na Real Sociedad wakati Real Madrid, walio Pointi 1 nyuma ya Barca na Atletico, pia watacheza Jumapili Ugenini na Athletic Bilbao.

Atletico na Real zina nafasi nzuri kuitungua Barca toka kileleni.
  
RATIBA/MATOKEO LA LIGA.


Barcelona 2 - 3 Valencia CF
    Levante 0 - 0 Rayo Vallecano
    Getafe 0 - 0 Real Valladolid

Position Team Played Goal Difference Points
1 Barcelona 22 43 54
2 Atlético Madrid 21 38 54
3 Real Madrid 21 39 53
4 Athletic Bilbao 21 14 42
5 Villarreal 21 17 37
6 Real Sociedad 21 12 36
7 Sevilla 21 5 31
8 Valencia CF 22 -4 28
9 Levante 22 -8 28
10 Espanyol 21 -2 26
11 Celta de Vigo 22 -6 25
12 Getafe 22 -12 25
13 Granada CF 22 -9 24
14 Osasuna 21 -16 22
15 Almería 21 -18 22
16 Málaga 21 -8 21
17 Elche 21 -13 21
18 Real Valladolid 22 -13 20
19 Rayo Vallecano 22 -30 17
20 Real Betis 21 -29 11


RATIBA/MATOKEO LA LIGA.
 

Jumapili Februari 2,2014.

Elche CF v UD Almeria
Real Betis v RCD Espanyol
Atletico de Madrid v Real Sociedad
Athletic de Bilbao v Real Madrid CF

Jumatatu Februari 3,2014.

Villarreal CF v Osasuna
  

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad