Azam FC na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Ferroviario de Beira Kombe la Shirikisho Afrika. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, February 09, 2014

Azam FC na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Ferroviario de Beira Kombe la Shirikisho Afrika.


Kipre Tchetche akimtoka beki wa kushoto wa Ferroviario, Emidio Matsinhe leo1-0 leo (Feb 09,2014) katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Awali Kombe la Shirikisho Afrika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam na Timu ya Azam FC kupata ushindi mwembamba wa bao 1-0.

Kiungo mkabaji wa Ferroviario, de Beira akipiga tik tak dhidi ya mshambuliaji wa Azam FC, Brian Umony leo(Februari 09,2014) Chamazi.
Wachezaji wa Azam wakimpongeza Kipre Tchetche ,mshambuliaji kutoka Ivory Coast,  aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 41 baada ya kutengewa pasi nzuri ya kichwa na Mganda Brian Umony na kufumua shuti kali.

Timu ya Azam FC imepata ushindi mwembamba wa bao 1-0, leo (Feb 09,2014) dhidi ya Ferroviario de Beira ya Msumbiji katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Awali Kombe la Shirikisho Afrika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaa.

Shukrani kwake mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 41 baada ya kutengewa pasi nzuri ya kichwa na Mganda Brian Umony na kufumua shuti kali.

Mchezo ulikuwa mkali dakika zote 90 na mashambulizi yalikuwa ya pande zote mbili.

Matokeo hayo yanamaanisha Azam FC itakuwa na kazi ngumu katika mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo nchini Msumbiji, wakitakiwa kulazimisha sare ili kusonga mbele.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad