Ushindi huo
wa awali uliwapa morari wachezaji hao na kufanya hadi mapumziko kutoka kifua
mbele kwa mabao 24-20.
Hadi mwamuzi anamaliza mchezo huo, Uganda ilikuwa kidedea kwa mabao 52-39 huku nahodha wao Peace akitwaa tuzo ya kuwa mfungaji bora wa michuano hiyo.
Kufuatia ushindi huo, Mwenyekiti wa Baraza la wawakilishi, Mgeni Hassani Juma aliipatia timu hiyo kombe la michuano hiyo.
Licha ya Uganda kutwaa ushindi huo, Tanzania Bara chini ya mfungaji wake Mwanaidi Hassan ilitwaa nafasi ya pili ya michuano hiyo.
Mchezaji Bora wa michuano hiyo ni Betina Kazinja kutoka Tanzania Bara, Mwajuma Hilika kutwaa mlinzi bora wa michuano hiyo.
![]() |
|
Peace
Proscovia akidaka mpira mbele ya wachezaji wa Tanzania Bara…katika Uwanja wa
Gymkhana, Zanzibar. Uganda iliifunga Tanzania Bara magoli 52-39.
|
![]() |
|
Mwanaidi
Hassan wa Tanzania Bara akidaka mpira pembeni ya wachezaji wa Uganda ambapo Uganda
iliifunga Tanzania Bara magoli 52-39.
|
![]() |
|
Sofia Komba
alicheza sana leo(Januari 11,2014) kujibu mapigo ya mpenzi wake, Joseph Owino
aliyeifungia Simba SC bao jana(Januari 10,2014) katika ushindi wa 2-0 kwenye soka dhidi ya URA
ya Uganda.
|
Aidha kwenye
soka ,Mechi za Nusu Fainali, Azam FC walinyang’anywa Taji walipotupwa nje ya
Mashindano ya Mapinduzi Cup, ambalo Mwaka huu ni kusheherekea Miaka 50 ya
Mapinduzi ya Zanzibar, baada kuchapwa 3-2 na KCC ya Uganda iliyotinga Fainali
na watakutana na Simba walioinyuka 2-0 URA ya Uganda.
Kwa Miaka
miwili iliyopita, Azam FC wamekuwa Mabingwa wa Mapinduzi Cup.
Simba
watacheza Fainali Jumatatu na KCC ambayo walikuwa nayo Kundi B kwenye
Mashindano haya na kutoka 0-0 katika Mechi yao.
FAINALI MAPINDUZI CUP 2014.
Jumatatu
Januari 13,2014.
Amaan
Stadium
SAA 10
JIONI: Simba SC v KCC












No comments:
Post a Comment