 |
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametangaza
kuwa leo, Jumatatu, Januari 13, 2014, itakuwa ni Siku ya Mapumziko (Public
Holiday) kwa Watanzania wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya
Zanzibar ya Januari 12,
mwaka 1964 yaliyofungua njia ya kuzaliwa kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
– miezi mitatu baada ya Mapinduzi hayo – Aprili 26, 1964.
|
 |
|
Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Ali Mohamed Shein
akikagua gwaride la heshima wakati wa kilele cha sherehe za miaka 50 ya
Mapinduzi ya Zanzibar ya Januari 12, mwaka 1964 katika Uwanja wa Amani Abeid
Karume Jana Januari 12, 2014.
|
 |
|
Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Ali Mohamed Shein
akikagua gwaride la heshima wakati wa kilele cha sherehe za miaka 50 ya
Mapinduzi ya Zanzibar katika Uwanja wa Amani Abeid Karume Jana Januari 12, 2014.
|
 |
|
Vijana
wakiachia njiwa kama alama ya amani wakati wa kilele cha sherehe za miaka 50 ya
Mapinduzi ya Zanzibar katika Uwanja wa Amani Abeid Karume Jana Januari 12, 2014.
|
 |
|
Rais Jakaya
Mrisho Kikwete na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mheshimiwa Ali Mohamed Shein wakimpongeza Rais Yoweri Kaguta Museveni
aliyeongea machache wakati wa kilele cha sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi ya
Zanzibar katika Uwanja wa Amani Abeid Karume leo Januari 12, 2014.
|
 |
|
Rais Jakaya
Mrisho Kikwete akimpongeza Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Ali Mohamed Shein kwa
hotuba nzuri aliyotoa wakati wa kilele
cha sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Uwanja wa Amani Abeid
Karume leo Januari 12, 2014.
|
 |
|
Rais Jakaya
Mrisho Kikwete na Rais Yoweri Kaguta Museveni wakiongea wakati wa kilele cha sherehe za miaka 50 ya
Mapinduzi ya Zanzibar katika Uwanja wa Amani Abeid Karume Jana Januari 12, 2014.
(PICHA NA
IKULU)
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametangaza
kuwa kesho, Jumatatu, Januari 13, 2014, itakuwa ni Siku ya Mapumziko (Public
Holiday) kwa Watanzania wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya
Zanzibar.
Rais Kikwete
ameutangaza uamuzi huo mjini Zanzibar ambako leo ameungana na Watanzania na
Wazanzibari wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya
Januari 12, mwaka 1964.
Mapinduzi
hayo yaliyoongozwa na mwasisi wa Zanzibar na Taifa la Tanzania, Hayati Abeid
Amaan Karume yalifanikiwa kuung’oa madarakani utawala dhalimu wa Sultan na
kuwawezesha kwa mara ya kwanza katika historia Waafrika walio wengine
kujitawala ndani ya nchi yao wenyewe.
Yalikuwa ni
Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofungua njia ya kuzaliwa kwa Muungano wa Tanganyika
na Zanzibar – miezi mitatu baada ya Mapinduzi hayo – Aprili 26, 1964.
Naye Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Ali Mohamed Shein
ametangaza kuwa kesho itakuwa Siku ya Mapumziko Tanzania Visiwani kusheherekea
miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Rais Shein
alitangaza mapumziko hayo wakati alipohutubia wananchi kwenye Uwanja wa Michezo
wa Amaan mjini Zanzibar katika kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi.
Imetolewa
na;
KURUGENZI YA
MAWASILIANO YA RAIS
Ikulu,
Dar es
Salaam.
Januari 12,
2014
No comments:
Post a Comment