SOMA:- uzembe, ikiwemo kulewa na kukaa juu ya reli, kuweka ‘headphone’ na kutembea relini kulivyosababisha watu 27 kupoteza maisha yao na wengine 27 wamejeruhiwa katika matukio yanayohusisha ajali za treni nchini mwaka 2013. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, January 04, 2014

SOMA:- uzembe, ikiwemo kulewa na kukaa juu ya reli, kuweka ‘headphone’ na kutembea relini kulivyosababisha watu 27 kupoteza maisha yao na wengine 27 wamejeruhiwa katika matukio yanayohusisha ajali za treni nchini mwaka 2013.

Gari aina ya Toyota Hilux lenye namba za usajili T697 BNB likiwa vibaya kutokana na kugonga treni ya abiria kwa mbele iliyokuwa ikitokea mikoa ya kanda ya ziwa… barabara ya iringa Dodoma (Picha na Maktaba yetu).


Asikari wa usalama barabarani akiwa karibu na Gari hilo baada yakuondolewa toka kwenye gema lililoinusuru isitumbukie chini ya Daraja ilipotokea ajali hiyo.

Muonekano wa Lori la kubeba mchanga likiwa limeharibika vibaya vibaya mara baada ya kuigonga treni ya mizigo katika eneo la Makulu mjini Dodoma ,ajali hiyo ilitokea baada ya lori hilo kukatiza reli katika sehemu ambayo haina kivuko na Hakuna aliyeumia katika ajali hiyo.
Kamanda wa Kikosi cha Reli Tanzania, Bi.Saada Haji anasema kwamba jumla ya ajali 79 zinazohusisha treni zilitokea mwaka jana(2013) katika mikoa tofauti nchini Tanzania. 



Alisema kuwa hata hivyo ajali nyingi kati ya hizo zimetokana na uzembe, ikiwemo kulewa na kukaa juu ya reli, kuweka ‘headphone’ na kutembea relini na madereva wa magari kukosa umakini wa kufuatilia alama za barabarani kwa kuendesha mwendo kati hata mahali penye kivuko cha treni. 

“ Treni linalofanya safari zake ndani ya jiji ndiyo ambalo kwa sasa linahisisha vifo vya watu wengi kwa muda mfupi tangu kuanza kwa safari zake watu 8 wamekufa huku wengine wakijeruhiwa,” alisema Kamanda Haji.

Alisisitiza” Hasa katika eneo la Daraja la Buguruni kwa Mnyamani ndiyo eneo ambalo ni hatari, kwani  limekuwa na matukio ya ajali, wananchi wengi hujisahau hukatiza juu ya reli kwa kuwa treni huwa halina breki za papo kwa papo basi vifo  au majeraha makubwa yanayowasababishia ulemavu wa kudumu,” 

Akizungumzia kuhusu matukio 285  ya uhalifu alisema kuwa yalitokea katika mikoa ya Morogoro, Dodoma, Itigi, Tabora, Mwanza, Kigoma, Mpanda  na Dar es Salaam, ambayo yaliyokea  katika maeneo ya reli na ndani ya treli. 

“ Polisi wa kikosi hiki wamekuwa wakipambana kikamilifu, kuna siku walifanikiwa kukamata mabegi yaliyowekea bangi, ambapo mtuhumiwa alifikishwa mahakamani ", alisema.

Alisema kuwa Polisi hao pia waliwahi kumbaini mhalifu mmoja aliyekuwa na amebeba silaha isivyo halali  ndani ya treni ambaye alikurupuka na kuitelekeza siraha hiyo

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad