Akitoa tathimini hiyo kwa waandishi wa habari mkoani Kigoma, Kamanda wa polisi mkoa wa Kigoma,Kamishina mwandamizi msaidizi wa polisi, SACP Frasser Kashai alisema sababu kubwa ya ongezeko la makosa yaliyoripotiwa ni uelewa wa wananchi wa jinsi ya kuripoti uhalifu na wahalifu na matokeo ya operation nyingi zilizofanyika kulinganisha na mwaka 2012
Alisema idadi ya watuhumiwa
waliokamatwa kwa makosa ya jinai katika kipindi cha Januari hadi disemba 27
mwaka 2013 imeongezeka mara tatu zaidi ambapo watuhumiwa 7,657 walikamatwa
ukilinganisha na watuhumiwa 2, 353 waliokamatwa kwa makosa hayo mwaka 2012.
Makosa yaliyotia fora mwaka 2013
ukilinganisha na mwaka 2012 ni kupatikana na silaha na unyang’anyi wa kutumia
silaha kosa ambalo linatokea zaidi maeneo ya vijiji vya mpakani mwa nchi jirani
ya Burundi huku matukio ya mauaji na ubakaji yakipungua.
Katika ripoti yake kamanda wa polisi
mkoani Kigoma, SACP Kashai alisema gram 810 za madawa ya kulevya aina ya
Cocaine,Bangi kilo 585.5, pombe haramu ya moshi lita 3,520 na mitambo 29 ya
kutengenezea Gongo vilakamatwa katika kipindi cha mwak 2013.
Idadi ya watuhumiwa waliokamatwa ni
514 ikilinganishwa na mwaka 2012 ambapo ilikamatwa pombe ya moshi lita 3,846 na
mitambo 22, Bangi kilo 792 na watuhumiwa 372 dhidi ya makosa hayo.
Idadi ya wahamiaji haramu
waliokamatwa mwaka 2013 imeongezeka ambapo jumla ya wahamiaji haramu 6,181
ikilinganishwa na wahamiaji haramu 598 waliokamatwa mwaka 2012.
Wahamiaji haramu waliokamatwa mwaka
2013 kati yao 5,135 ni kutoka nchini Burundi, 1,045 kutoka Jamhuri ya
kidemokrasia ya watu wa Congo DRC na 1 kutoka Rwanda 1 hivyo kuwepo ongezeko la
ukamataji wa wahamiaji haramu 5,583 katika mkoa wa Kigoma.
Aidha kamanda Kashai alitaja matokeo
ya makosa makubwa na madogo na hatua zilizofikiwa ukilinganisha na mwaka jana
kuwa waliohukumiwa mwaka 2013 kwa makosa makubwa ni watu 201 ikilinganishwa na
watu 310 mwaka 2012.
Kesi zilizofungwa na Polisi mwaka
2013 ni 346 ikilinganishwa na kesi 388 mwaka jana, Kesi zilizoko mahakamani
mwaka 2013 ni 1,170 ikilinganishwa na kesi 966 mwaka jana.
Zilizoshindwa mahakamani ni kesi 124
ikilinganishwa na kesi 57 mwaka jana wakati zilizoko mahakama kuu ni kesi 22
ikilinganishwa na kesi 9 za mwaka jana.
Makosa madogo waliohukumiwa ni watu
1,052 mwaka 2013 ikilinganishwa na watu 1,414 mwaka jana. Kesi zilizofungwa na
polisi mwaka 2013 ni 3,407 ikilinganioshwa na 4,463 mwaka jana, zilizoko
mahakamani mwaka jana zilikuwa kesi 1,383 na mwaka 2013 ni kesi 1,052.
Upande wa makosa ya usalama
barabarani kamanda Kashai alisema jeshi la polisi mkoani Kigoma kupitia kikosi
cha usalama barabarani katika kipindi cha mwaka 2013 limekamata jumla ya makosa
12,987 ikilinganishwa na makosa kama hayo 10,920 yaliyokamatwa mwaka jan.
Kati ya hayo makosa 12,917 yalitozwa
faini na kuiingizia serikali kiasi cha shilingi milioni 387.5 ikilinganishwa na
mwaka jana ambapo makosa 10,870 yaliyotozwa faini yaliingizia serikali kiasi
cha shilingi milioni 326, ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 19%.
Aidha alisema ajali za barabarani
zilipungua kwa asilimia 7% kutoka ajali 289 mwaka jana hadi kufikia ajali 268
mwaka 2013 huku makosa makubwa yaliyoripotiwa kusababisha vifo na majeruhi ni 140 ambapo kutokana na makosa hayo kesi
127 zilipelekwa mahakamani na zilizotolewa hukumu ni kesi 55 na kesi 72 bado
hazijatolewa hukumu.
Takwimu hizo zimetaja kuwepo kwa
ongezeko la watu waliofariki kwa ajali za barabarani kwa asilimia 31% ambapo
mwaka 2013 kuna vifo 102 ikilinganishwa na mwaka jana watu 78 na kuna ongezeko
la majeruhi kwa asilimia 26% kutoka majeruhi 57 mwaka jana hadi kufikia
majeruhi 279 mwaka 2013.
Kuhusu matukio ya ajali za Pikipiki
kwa mwaka 2013 kamanda Kashai alisema kulikuwepo na ajali 58 zilizosababishwa
na pikipiki ambapo jumla ya pikipiki 77 zilihusika na katika ajali hizo wapanda
pikipiki 24 walipoteza maisha na wapanda pikipiki 33 walijeruhiwa.





No comments:
Post a Comment