Serikali ya Tanzania yatoa zaidi ya Shilingi milioni 45 kwa ajili ya ununuzi wa mashine mpya ya kusukuma maji katika mji wa Ngara mkoani Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, November 30, 2013

Serikali ya Tanzania yatoa zaidi ya Shilingi milioni 45 kwa ajili ya ununuzi wa mashine mpya ya kusukuma maji katika mji wa Ngara mkoani Kagera.

Mwenye shati la Kijani  ni Bw.Issa Samma(MMEC-Ngara),Bw.John Shimilimana(Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara na Diwani wa Kata ya Kibimba,Waziri wa nchi Ofisi ya Rais, Mahusiano na Utaribu Bw Steven Wasira, na kushoto kwake ni Mkuu wa wilaya ya Ngara Mkoani Kagera Bw Costantine Kanyasu, wote walifuatana na Waziri Wasira  kijini Ibuga kata ya Kabanga-Ngara kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo katika ziara ya Waziri Wasira ya kikazi ya siku moja (Novemba 28,2013) Wilayani Ngara.
Serikali ya Tanzania imetoa zaidi ya Shilingi  milioni 45 kwa ajili ya ununuzi wa mashine mpya ya kusukuma maji ikiwa ni jitihada za serikali katika kutatua tatizo la maji katika mji wa Ngara mkoani Kagera.

Mkuu wa wilaya ya Ngara Bw Costantine Kanyasu amemueleza waziri wa nchi ofisi ya rais, Mahusiano na Uratibu Bw Steven Wasira kuwa mji wa Ngara umekuwa na tatizo kubwa la maji hali inayosababisha wakazi wa mji huo kukosa maji kwa kipindi cha hadi wiki mbili.

Amesema kuwa tatizo hilo lilifikishwa kwa Rais wa Tanzania Dr. Jakaya Kikwete alipofanya ziara wilayani  humo hivi karibuni, hali iliyosaidia kupatikana kwa Shilingi milioni 45 kwa ajili ya kusaidia kutatua tatizo hilo.

Kwa upande wake Waziri Wasira amesema kuwa maeneo mengi ya nchi yanakabiliwa na uhaba wa maji na kwamba ili kutatua tatizo hilo kuna haja ya kuibuliwa chanzo kipya cha maji pamoja na kuwepo kwa umeme wa uhakika kwenye maeneo yenye mitambo ya maji.

Aidha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa Serikali yake itaongeza kwa kiasi kikubwa kasi ya kusambaza huduma za umeme na maji katika vijiji nchini kwa nia ya kuboresha maisha ya wananchi na kwamba katika kipindi cha mwaka mmoja ujao, Serikali yake inatarajia kusambaza huduma ya maji katika vijiji 1,449 katika hatua inayokadiriwa kuwa itawanufaisha watu wapatao milioni saba.


Source:-Radio Kwizera-Ngara.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad