Kwenye Mechi
ya Zanzibar na Ethiopia, Bao za Wahabeshi zilifungwa na Fasika Asfan, Dakika ya
5, Salahadin Bargicho, kwa penalti ya Dakika ya 37, na Yonathan Kebede kuingiza
Bao la 3 katika Dakika ya 83.
Bao la
Zanzibar lilifungwa na Awadh Juma Issa katika Dakika ya 68.
Katika Mechi
iliyofuatia, Wenyeji Kenya walitangulia kufunga Bao katika Dakika ya 16 kwa
Penati ya Joackins Atudo lakini South Sudan ilisawazisha katika Dakika ya 26
kwa Bao la Richard Jistin.
Katika
Dakika ya 29, Jacob Keli aliifungia Kenya Bao la Pili na katika Dakika ya 70,
Atudo alikosa kufunga Penati ambayo Kipa wa South Sudan aliokoa lakini Kenya
wakapata Bao lao la 3 alilofunga David Owino katika Dakika ya 78.
Ushindi huo unaifanya Harambee Stars ifikishe pointi nne baada ya awali kutoa sare ya bila kufungana na Ethiopia katika mchezo wa ufunguzi.
Matokeo haya
yanamaanisha Kenya na Ethiopia sasa zinalingana kwa kila kitu, pointi nne kila
mmoja, mabao matatu ya kufunga na bao moja la kufungwa, wakati Zanzibar sasa ni
ya tatu kwa pointi zake tatu na Sudan Kusini inashika mkia.
Jumapili (Desemba 01,2013) zipo Mechi 2 za Kundi B katika ya Kilimanjaro Stars na Somalia na Zambia watacheza na Burundi, Mechi zote zikiwa huko Nairobi Uwanja wa Nyayo.






No comments:
Post a Comment