Akizungumza
na waandishi wa habari jana, Ofisa Upelelezi Makosa ya Jinai (RCO), ambaye pia
ni Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Joseph
Konyo, alisema watuhumiwa walikamatwa baada ya kufuatiliwa na polisi.
Watuhumiwa
hao (majina yanahifadhiwa)
wenye
umri wa miaka 36 na 43
(ni
waganga wa jadi wawili) na
mfanyabiashara
ana miaka 48.
|
"Oktoba
20 mwaka huu, tulipata taarifa za mtu mmoja kujihusisha na biashara ya viungo
vya binadamu, eneo la Igombe, Manispaa ya Ilemela...tulimtuma mtu wetu ili
akafanye manunuzi ya viungo hivyo, kutoka kwa mganga mmoja (jina linahifadhiwa).
"Hivi
karibuni tulifanya vikao na waganga wa jadi kuzungumzia umuhimu wa kushirikiana
na kupeana taarifa za kubaini waganga wanaopiga ramli chonganishi na wakata
mapanga lengo likiwa ni kukomesha mauaji ya vikongwe," alisema.
Alisema
baada ya vikao hivyo, walipokea taarifa kuwa mganga wa jadi huko Igombe anauza
viungo vya binadamu na kuweka muda maalumu wa kutoa kichwa cha binadamu, mkono,
nyeti.
Mganga huyo
alizungumza na mteja (polisi), wakutane ili wafanye biashara akidai yupo na
wenzake wawili wakiwa na begi ambapo mganga huyo alitaka apewe sh. milioni 100
lakini mteja aliomba apunguziwe bei na kuwaweka watu hao chini ya ulinzi.
"Baada
ya begi lao kupekuliwa, kulikutwa chungu ambacho ndani yake kulikuwa na mfuko
wa plastiki uliokuwa na kiganja cha mkono wa kuume wa binadamu kikiwa
hakijaharibika.
Konyo
alikataa kutaja majina ya watuhumiwa kwa madai ya kuvuruga upelelezi, kwani
bado wanamtafuta mfanyabiashara mmoja jijini humo ambaye ametajwa na watuhumiwa
kuwa anajihusisha na biashara hiyo.








No comments:
Post a Comment