![]() |
Said
Ndemla akimpongeza
Mombeki baada ya kufunga.
|
Wekundu wa
Msimbazi Simba SC imezinduka jioni ya leo(November 06,2013) baada ya kucheza
mechi nne bila kushinda, ikiibuka na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Ashanti United
ya Ilala, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara.
Simba SC
kumbuka ilitoka sare tatu dhidi ya Yanga SC
(3-3), Coastal Union (0-0) na Kagera Sugar (1-1) na kufungwa 2-1 na Azam
FC.
Simba SC leo
ilipata ushindi wake kupitia kwa Betram Mombeki aliyefunga mawili, Amisi Tambwe
na Ramadhani Singano ‘Messi’.
Pamoja na
ushindi huo, Simba SC inabaki nafasi ya nne kwa pointi zake 24, baada ya
kucheza mechi zote 13 za mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu.
Azam FC na
Mbeya City zina pointi 26 kila moja na Yanga inafuatia kwa pointi zake 25 na
timu zote hizo zitacheza mechi zake za mwisho kesho(November 07,2013).
Katika
mchezo huo uliochezeshwa na refa Andrew Shamba wa Pwani, hadi mapumziko tayari
timu hizo zilikuwa zimekwishafungana bao 1-1.
Simba SC
walitangulia kupata bao dakika ya nane kupitia kwa winga wake machachari,
Ramadhani Singano ‘Messi’ aliyepasua katikati ya ukuta wa Ashanti baada ya pasi
ya Amisi Tambwe kabla ya kumchambua kipa mkongwe, Amani Simba.
![]() |
Mshambuliaji
wa Simba SC, Amisi Tambwe akimtoka beki wa Ashanti United, Hussein Mkongo jioni
ya leo (November 06,2013) Taifa.
|
Ashanti walisawazisha
dakika ya 45 mfungaji, Hussein Swedi aliyeunganisha kwa kichwa krosi maridadi
ya Hussein Mkongo kutoka wingi ya kulia.
Keshokutwa
(Novemba 7 mwaka huu) raundi ya 13 kumaliza mzunguko wa kwanza itakamilika kwa
mechi kati ya Yanga na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa kwa viingilio vya sh.
5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.
Azam itakuwa
mwenyeji wa Mbeya City kwenye Uwanja wa Chamazi wakati Uwanja wa Ali Hassan
Mwinyi mjini Tabora utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Rhino Rangers na Tanzania
Prisons kutoka Mbeya.
Novemba 7
mwaka huu, Azam itacheza na Mbeya City, Yanga itacheza na Oljoro JKT kwenye
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Rhino itakuwa mwenyeji wa Tanzania
Prisons.
MATOKEO:-Jumatano
Novemba 6,2013.
JKT Ruvu 1
Coastal Union 0
Ashanti
United 2 Simba 4
Kagera Sugar
2 Mgambo Shooting 0
Ruvu
Shooting 2 Mtibwa Sugar 2
RATIBA:-Alhamisi
Novemba 7,2013.
Azam FC v
Mbeya City
Yanga v JKT
Oljoro
Rhino
Rangers v Tanzania Prisons
MSIMAMO VPL 2013/2014.
NO
|
TEAMS
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
PTS
|
1
|
Azam FC
|
12
|
7
|
5
|
0
|
20
|
7
|
13
|
26
|
2
|
Mbeya City
|
12
|
7
|
5
|
0
|
17
|
8
|
9
|
26
|
3
|
Young Africans
|
12
|
7
|
4
|
1
|
28
|
11
|
17
|
25
|
4
|
Simba SC
|
13
|
6
|
6
|
1
|
26
|
13
|
13
|
24
|
5
|
Kagera Sugar
|
13
|
5
|
5
|
3
|
15
|
10
|
3
|
20
|
6
|
Mtibwa Sugar
|
13
|
5
|
5
|
3
|
19
|
17
|
2
|
20
|
7
|
Ruvu Shootings
|
13
|
4
|
5
|
4
|
15
|
15
|
0
|
17
|
8
|
Coastal Union
|
13
|
3
|
7
|
3
|
10
|
7
|
3
|
16
|
9
|
JKT Ruvu
|
13
|
5
|
0
|
8
|
10
|
16
|
-6
|
15
|
10
|
Rhino Rangers
|
12
|
2
|
4
|
6
|
9
|
16
|
-7
|
10
|
11
|
JKT Oljoro
|
12
|
2
|
4
|
6
|
9
|
16
|
-7
|
10
|
12
|
Ashanti United
|
13
|
2
|
4
|
7
|
12
|
24
|
-12
|
10
|
13
|
Tanzania Prisons
|
12
|
1
|
5
|
6
|
6
|
16
|
-10
|
8
|
14
|
Mgambo JKT
|
13
|
1
|
3
|
9
|
3
|
23
|
-20
|
6
|







No comments:
Post a Comment