Bao 2 za Aaron Ramsey na moja la Mathieu Flamini zimewapa Arsenal ushindi wa Bao 3-0 walipocheza Ugenini na Cardiff City. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, November 30, 2013

Bao 2 za Aaron Ramsey na moja la Mathieu Flamini zimewapa Arsenal ushindi wa Bao 3-0 walipocheza Ugenini na Cardiff City.



Mchezaji Ramsey hakutaka kushangilia baada ya kuifunga timu yake ya zamani ya Cardiff City lakini sasa Arsenal imezidi kijichimbia kileleni mwa Ligi Kuu ya England, na Ushindi huo wa bao 3-0 unaifanya Arsenal itemize pointi 31 baada ya kucheza mechi 13, ikiizidi Liverpool iliyo katika nafasi ya pili kwa pointi saba.
LIGI KUU ENGLAND RATIBA/MATOKEO.
Jumamosi Novemba 30,2013.

Aston Villa 0 Sunderland 0
Cardiff 0 Arsenal 3
Everton 4 Stoke 0
Norwich 1 Crystal Palace 0
West Ham 3 Fulham 0


EVERTON 4 - 0 STOKE

Bao za Deulofeu, Coleman, Oviedo na Lukaku, leo zimewapeleka Everton juu na kukamata Nafasi ya 4 katika Msimamo wa Ligi Kuu England walipoibwaga Stoke City Bao 4-0 Uwanjani Goodison Park.

WEST HAM 3 -0 FULHAM 

 Sasa, bila shaka, Meneja wa Fulham, Martin Jol, yuko hatarini kumwaga unga  baada ya Timu yake kuchapwa Bao 3-0 na West Ham walipocheza Ugenini Uwanja wa Upton Park.

Bao za West Ham zilifungwa na Diame, Carlton Cole na Joe Cole.

CARDIFF CITY 0 - 3 ARSENAL 

Bao 2 za Aaron Ramsey na moja la Mathieu Flamini zimewapa Arsenal ushindi wa Bao 3-0 walipocheza Ugenini na Cardiff City.

Ushindi huu umewafanya Arsenal wazidi kupaa kileleni wakiwa Pointi 7 mbele.

NORWICH 1 - 0 CRYSTAL 

Bao la Dakika ya 30 la Gary Hooper, limewapa Norwich City ushindi wa Bao 1-0 walipocheza na Crystal Palace waliokuwa na Menja mpya Tony Pulis ambae leo ndio rasmi alikuwa akianza kazi.

Kipigo hichi kimewabakisha Palace mkiani na Norwich kupanda hadi Nafasi ya 14.

LIGI KUU ENGLAND RATIBA.
[Saa za Bongo]
Jumapili Desemba 1,2013.

15:00 Tottenham v Man United
17:05 Hull v Liverpool
19:10 Chelsea v Southampton
19:10 Man City v Swansea

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad