Baada ya Mafunzo ya ufundi katika Chuo cha Ufundi Ilemela wilayani Muleba,Vijana wapatiwa Vifaa vya kuanza Maisha ili Kujitegemea. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, November 07, 2013

Baada ya Mafunzo ya ufundi katika Chuo cha Ufundi Ilemela wilayani Muleba,Vijana wapatiwa Vifaa vya kuanza Maisha ili Kujitegemea.

Muonekano wa  Vijana 22 wa fani ya useremala na ushonaji waliohitimu mwaka huu katika  chuo cha ufundi  Ilemela wilayani Mulena mkoani Kagera ambao wamepatiwa msaada wa vitendea kazi vyenye thamani ya shilingi Milioni mbili ili kuanza maisha ya kujitegemea kutoka Kanisa la KKKT Ilemela wilayani Muleba mkoani Kagera (Novemba 02,2013).Habari/Picha na Shaaban Ndyamukama.



Baadhi ya Vifaa vya useremala  vilivyotolewa kwa ajili ya Vijana  waliohitimu mwaka huu katika  chuo cha ufundi  Ilemera wilayani Mulena mkoani Kagera.

Juu na Chini Ni kikundi cha Ngoma za asili (Akasimbo) kutoka Kijiji cha Rulanda wilayani Muleba kikitumbuiza katika mahafali ya kuhitimu  Vijana 22 wa fani ya useremala na ushonaji kwa mwaka huu katika  chuo cha ufundi  Ilemela wilayani Mulena mkoani Kagera. 


Kutoka kushoto ni Mkuu wa Chuo Bw.Jofrey T.Erenest wanaofatia ni Bw.Olson Barbro na Mkewe ambao nio wafadhiri wa Vifaa vya Ushonaji na Useremala,Mchungaji wa KKKT -Phinias Rwakatare pamoja na Askofu wa KKKT Elias Buberwa.


Ni kikundi cha Ngoma za asili (Akasimbo) kutoka Kijiji cha Rulanda wilayani Muleba kikitumbuiza katika mahafali ya kuhitimu  Vijana 22 wa fani ya useremala na ushonaji kwa mwaka huu katika  chuo cha ufundi  Ilemela wilayani Mulena mkoani Kagera(Novemba 02,2013). 
Jumla ya Vijana 22 wa fani ya useremala na ushonaji waliohitimu mwaka huu katika  chuo cha ufundi  Ilemera wilayani Mulena mkoani kagera wamepatiwa msaada wa vitendea kazi vyenye thamani ya shilingi Milioni mbili ili kuanza maisha ya kujitegemea.

Mkuu wa chuo hicho  Bw Geoffrey  Ernest Tilwetwa   amebainisha hayo wakati wa mahafali ya tano ya wahitimu wa fani ya ufundi chuoni hapo na kwamba msaada huo umetolewa na mfadhili wa chuo mchungaji Olsson Barbro kutoka Sweeden.

Bw Tilwetwa amesema amesema kuwa wasichana wamepatiwa vyerehani pamoja  na vifaa vya ushonaji vyenye thamani ya shilingi 600,000/= huku wavulana wakipatiwa zana za useremala zenye thamani ya shilingi 700,000/=.

Aliongeza kuwa wavulana waliongezewa  na fedha taslimu Tsh.50,000/=   kwa ajili ya kujinunulia mbao ili kutengeneza  samani za mfano kwa wateja.

Ameongeza kuwa katika kuwafadhili zana hizo uongozi wa chuo na kanisa huwatembelea vijana kwenye familia  zao  mara  nne kwa mwaka kujionea maendeleo yao na changamoto zinazowakabili kisha kutoa ushauri wa kufanikisha maisha yao.

“Pamoja na juhudi hizo bado chuo hiki tangu kianza mwaka 2002 kinakabiliwa na tatizo la ukosefu wa umeme kurahisisha ufundishaji wa nadharia na vitendo pamoja na bweni la wanafunzi”.Alisema.

Hata hivyo amewaasa vijana hao kutodharau kazi katika maisha yao na kuhakikisha vifaa walivyopewa vinatunzwa na kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa kwa matendo na kutumia maadili ya kanisa kuwa watumishi bora mbele ya Mungu.

Wakisoma risala mbele ya baba askofu wa KKKTdayosisis ya kaskazini magharibi mkoani Kagera mhashamu Elisa Buberwa wahitimu hao licha ya kushukuru walimu wao kwa mafunzo na kufadhiliwa vitendea kazi wameomba chuo hicho kuondolewa na changamoto zilizopo.

Wamesema chuo hicho na wanachuo wanaoendelea kupata fani ya useremala na ushonaji wanahitaji kupatiwa mavazi ya kikazi (Overall) kwa  wavulana ikiwa ni pamoja na bweni lao,kuongeza matundu ya vyoo ,kuwa na gari la kituo  na mlinzi kupatiwa baiskeli ili kutekeleza vema majukumu yake.


Hata hivyo Mwenyekiti wa Ilemera Carpentry  Centre for Ophance (ICCO) mchungaji Phinias  Rwakatale wa jimbo la kusini B  ilemera  amewahimiza vijana kuwa na uaminifu katika kazi zao ili waweze kukubalika ndani ya jamii zao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad