Baada ya ngome za M23 mashariki mwa DRC kusambaratishwa, Kiongozi wa kijeshi wa kundi hilo Sultani Makenga ajisalimisha kwa jeshi la Uganda. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, November 07, 2013

Baada ya ngome za M23 mashariki mwa DRC kusambaratishwa, Kiongozi wa kijeshi wa kundi hilo Sultani Makenga ajisalimisha kwa jeshi la Uganda.

Kiongozi wa kijeshi wa kundi la M23, Sultani Makenga
REUTERS/James Akena.
Duru sahihi kutoka katika jeshi la Uganda zimearifu kwamba Makenga amejisalimisha akiwa na wapiganaji zaidi ya 1500 katika eneo la mpaka wa DRC na Uganda.

Msemaji wa jeshi la serikali ya Uganda Paddy Ankunda hapo awali alifahamisha kuwa wapiganaji 1500 wa kundi la M23 wamejisalimisha mikononi mwa jeshi lao pamoja na Sultani Makenga, ingawa hakusema lolote juu ya hatma ya kamanda huyo.


Kujisalimisha kwa wapiganaji hao kunakuja wakati huu ambapo Umoja wa Mataifa UN umeahidi kuendelea kuisaidia serikali ya DRC kuimarisha usalama wa mipaka yake baada ya kufanikiwa kusambaratisha ngome zote za waasi wa M23 mashariki mwa nchi hiyo.

Mkuu wa vikosi vya Umoja wa Mataifa nchini DRC, MONUSCO, Martin Kobler amethibitisha vikosi vyao vitaendelea kuweka kambi karibu na mpaka ili kudhibiti upitishwaji wa silaha na kukabiliana na wapiganaji wa Kihutu wa FDLR wanaingia nchini Rwanda.

Majeshi ya serikali ya DRCongo yakiungwa mkono na brigedi maalumu ya UN juma hili yalifanikiwa kuwazidi nguvu waasi wa M23 ambao walianza harakati zao mwanzoni mwa mwaka 2012.

Wakati hayo yakijiri serikali ya Jamhuri ya Kinshasa imesema kuwa itatia saini azimio la amani na kundi la waasi wa M23 na si mkataba wa kusitisha vita dhidi ya kundi hilo iwapo litaendelea na uasi mashariki mwa nchi hiyo.

Kauli hiyo imetolewa na msemaji wa serikali, Lambert Mende ambaye amesisitiza kuwa azimio litakalotiwa saini ni la kusitisha vita kwa muda.

Kwa upande wao kundi la waasi wa M23 kupitia kwa mpatanishi wake kwenye mazungumzo ya kampala, Roger Lumbala anasema kuwa kwa sasa kundi lao litageuzwa na kuwa chama cha siasa na kwamba serikali lazima itekeleze maazimio ya jumuiya ya kimataifa.


Naye mwakilishi maalumu wa UN, Mary Robinson ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa UNSC kuwa ushindi dhidi ya M23 ni muhimu katika wakati huu ambapo jitihada za kutokomeza uasi mashariki mwa DRC zikizendelea.

Chonzo:-rfi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad