Tazama taswira ya kumalizika kwa Mashindano ya Millenium Cup 2013 Kata ya Bugarama wilayani Ngara mkoani Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, October 01, 2013

Tazama taswira ya kumalizika kwa Mashindano ya Millenium Cup 2013 Kata ya Bugarama wilayani Ngara mkoani Kagera.

Katika Utoaji wa Zawadi hizo Mshindi wa tatu katika soka ilikuwa timu ya Rwinyana, Kihinga walikuwa washindi wa pili huku mshindi wa kwanza na timu yenye nidhamu iliyotoa na mchezaji bora ikiwa ni Bukiriro FC.
Habari/Picha na Shaaban Ndyamukama.















Zawadi zilizotolewa ni kwa  washindi wa kuvuta kamba Kihinga  na Rwinyana kwa kupata elfu 20 kila timu , mshindi wa kukimbia na chupa ya maji kichwani na kukalia  kiti baada ya kukizunguka Elida Mose maarufu kwa kuitwa Mama Deusi  alipata nguo aina vitenge viwili  na  Salome Emanuel kujinyakulia  pair ya khanga. 
Mashindano ya Millenium Cup 2013 yaliyoanza mwezi Agost mwaka huu katika kata ya Bugarama wilayani Ngara mkoani Kagera yamehitimishwa mwishoni mwa wiki (Septemba 29,2013) kwa washiriki kujinyakulia zawadi mbalimbali.

 Mashindano hayo yalijumuisha michezo ya kuvuta kamba kufukuza kuku kulenga shabaha mpira wa soka na michezo mingineyo kwa kushirikisha timu za kijiji cha Rwinyana ,Bugarama, Mumiramira,Kihinga na Bukiriro ambapo aliyefunga mashindano hayo ni  Afisa Tawala wilayani Ngara ,Davidi Mafipa.

Zawadi zilizotolewa ni kwa  washindi wa kuvuta kamba Kihinga  na Rwinyana kwa kupata elfu 20 kila timu , mshindi wa kukimbia na chupa ya maji kichwani na kukalia  kiti baada ya kukizunguka Elida Mose maarufu kwa kuitwa Mama Deusi  alipata nguo aina vitenge viwili  na  Salome Emanuel kujinyakulia  pair ya khanga.


Katika Utoaji wa Zawadi hizo Mshindi wa tatu katika soka ilikuwa timu ya Rwinyana, Kihinga walikuwa washindi wa pili huku mshindi wa kwanza na timu yenye nidhamu iliyotoa na mchezaji bora ikiwa ni Bukiriro FC.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad