Serikali wilayani Ngara mkoani Kagera yakanusha Mauaji ya watu wawili yaliyotokea katika kijiji cha Kasulo wilayani humo, yalitekelezwa kwa shinikizo la viongozi ngazi ya Wilaya pamoja na Mkoa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, October 01, 2013

Serikali wilayani Ngara mkoani Kagera yakanusha Mauaji ya watu wawili yaliyotokea katika kijiji cha Kasulo wilayani humo, yalitekelezwa kwa shinikizo la viongozi ngazi ya Wilaya pamoja na Mkoa.

Mkuu wa wilaya ya Ngara,
 Bw Costantine Kanyasu
Akiongea na wandishi wa
Habari leo (Octoba 01,2013) ofisini kwake.
Serikali wilayani Ngara mkoani Kagera imekanusha taarifa zilizotolewa katika vyombo vya habari kuwa kuna Mauaji ya watu wawili yaliyotokea katika kijiji cha Kasulo wilayani humo, yalitekelezwa kwa shinikizo la viongozi ngazi ya wilaya pamoja na Mkoa.

Mkuu wa wilaya ya Ngara, Bw Costantine Kanyasu  ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama ,amesema hayo leo (Octoba 01,2013) ofisini kwake wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu taarifa  zilizotolewa hivi karibuni.

Bw. Kanyasu amesema kuwa mauaji ya watu hao yalitekelezwa na watu 15 wakiongozwa na mmoja wao anayejiita Mwanaharakati ambaye kwa sasa pamoja na wenzake wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa hatua zaidi za Kisheria.

Amesema kuwa katika mauaji hayo ni Ng’ombe 17 waliuawa na Wananchi na sio ng’ombe  300 kama ilivyodaiwa na baadhi ya vyombo vya habari kwa kusikiliza mawazo ya Wananchi bila kuthibitishwa na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Ngara.

Mkuu wa wilaya ya Ngara,
 Bw Costantine Kanyasu.
Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa wilaya ya Ngara ,Mkoani Kagera ametoa wito kwa Wananchi kuepuka kujichukulia sheria mkononi  hasa kwa kuwaondoa Wahamiaji  wanaoishi Wilayani  humo  kinyume cha sheria kwani jukumu hilo linasimamiwa na kikosi maalumu cha Operasheni kimbunga awamu ya pili.
Bw.Kanyasu ametoa wito kuwa wananchi wasiendelee kuwakaribisha wahamiaji katika maeneo yao hasa vijijini ikiwa ni pamoja na kuwapatia maeneo ya kufugia kwani mazingira yote yamejaa nani kwa ajili ya Wananchi wa Ngara kwa shughuli zao za Kimaendeleo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad