Rusumo FC ni Bingwa wa Brayan Cup 2013 kwa kuwazibua Mabingwa wa wilaya ya Ngara na Polisi Jamii Murusagamba FC. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, October 01, 2013

Rusumo FC ni Bingwa wa Brayan Cup 2013 kwa kuwazibua Mabingwa wa wilaya ya Ngara na Polisi Jamii Murusagamba FC.

Muonekano wa zawadi za Ngao na fedha tasilimu Laki 7 zilizotolewa kwa Mshindi wa kwanza hadi wa tatu pamoja na timu yenye nidhamu,mchezaji bora  na Mfungaji bora wa BRAYAN CUP 2013.

 Mabingwa wa Wilaya ya Ngara na Kombe la Polisi Jamii Timu ya Murusagamba FC wakiwa uwanjani kabla ya mchezo wao na Rusumo FC wakati wa Mgeni rasmi Mjumbe wa CCM -NEC Taifa wilaya ya Ngara Issa Samma akiwapa nasaha  ya kucheza kwa upendo na nidhamu katika mchezo huo wa fainali ya Brayan Cup -Setemba 29,2013.

 Kikosi cha  Rusumo FC  kikiwa uwanja wa Kokoto mjini Ngara ambapo kilichuana na Mabingwa wa Wilaya ya Ngara na Kombe la Polisi Jamii Timu ya Murusagamba FC na kuwafunga kwa bao 1-0.


Mgeni rasmi Mjumbe wa CCM -NEC Taifa wilaya ya Ngara Issa Samma katikati akimsikiliza Mwl.Godfrey Brayan muandaaji wa Mashindano hayo kushoto wakati wa kutoa hatuba yake huku kulia kwake ni Diwani wa Kata ya Ngara Mjini CCM Charles Rujuba.

Mwandishi wa habari za Michezo na Burudani wa radio kwizera FM Boaz Zobanya akichukua sehemu ya matukio kwa kumrekodi Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Brayan Cup 2013 na Kaimu Katibu mkuu wa chama cha soka wilaya ya Ngara NDFA - Bahati Kunzi.

Baadhi ya wachezaji wa Mabingwa wa kombe la Brayan CUP 2013-Rusumo FC wakisubili kukabidhiwa zawadi zao na Mgeni rasmi Mjumbe wa CCM -NEC Taifa wilaya ya Ngara Issa Samma mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa fainali ya Brayan Cup -Setemba 29,2013 katika uwanja wa kokoto Mjini Ngara.
Viongozi wa Kada mbalimbali na wadau wa Michezo wilayani Ngara mkoani Kagera wametakiwa kushimakama kwa pamoja ili kuendeleza sekta ya Michezo wilayani humo.

Akihitimisha mashindano ya kuwania Kombe la  Brayan kwa mwaka huu, Mjumbe wa CCM-NEC Taifa wilaya ya Ngara mkoani Kagera na Mdau mkubwa wa michezo Issa Samma amesema kuwa kwa kupitia mashindano hayo ya BRAYAN CUP 2013, yaliyohitimishwa  Septemba 29,2013 katika uwanja wa Kokoto mjini Ngara-hawana budi kujitoa kwa nia ya dhati ili kuleta maendeleo ya michezo pamoja na vipaji vya wachezaji.

Issa Samma aliwataka Viongozi na Wadau kujiuliza kwa nini (Why not Me) wanashindwa kuendeleza michezo mbalimbali wilayani sambamba na kuanzisha Mashindano ili kuleta hamasa ya Michezo.

Kwa upande wake Muandaaji wa Kombe hilo la Brayan-Mwl.Godifrey Brayan licha ya kutangaza kuwa kombe hilo litakuwa likishindaniwa kila mwaka,amewashukuru wadau na wananchi wa wilaya ya Ngara kwa kuzisaidia timu 12 zilizoshiriki kwa hali na mali  mashindano hayo kwa mwaka huu.

Pia alishauri Viongozi wa Michezo na Wadau kuacha kuendekeza Majungu na Vikwazo kwa wadau wanaojitokeza kuendeleza michezo.

Awali mwenyekiti wa kamati ya mashindano hayo Bahati Kunzi alisema mashindano hayo yalikumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo Kukosekana kwa Waamuzi wa kutosha na waliofuzu Mafunzo ya Uamuzi,Kutokuwepo kwa Viwanja Bora na Vinavyokidhi Viwango vya FIFA pamoja na Elimu ndogo ya Uelewa wa masuala ya Mpira wa miguu hususani kwa Mashabiki jambo ambalo linaweza kuleta vurugu uwanjani.

Katika fainali hiyo Timu ya Rusumo FC ilifanikiwa kuibuka Bingwa wa kombe hilo kwa kuwafunga Mabingwa wa Wilaya ya Ngara na Kombe la Polisi Jamii Timu ya Murusagamba FC kwa bao 1-0 na hivyo kujiondokea na fedha tasilimu shilingi Laki 3 na Ngao.

Mshindi wa pili Murusagamba FC aliondoka na shilingi Laki 2 na Ngao huku mshindi wa tatu Walimu FC wakiondoka na Ngao na shilingi Laki Moja.

Timu yenye nidhamu Rusumo FC iliondoka pia na shilingi Elfu 40,Mfungaji bora Inocent Buninange kutoka Rusumo FC akiweka shilingi Elfu 30 huku Mchezaji bora Musa John kutoka Walimu FC na Baraka Nelson kutoka Ngara Starz wakiondoka na shilingi Elfu 15 kila mmoja.

Timu 12 zilizoshiriki Brayan Cup kwa mwaka huu ni Rusumo FC ,Mtoni FC,Boda boda FC,Benaco FC,Nyakisasa FC,Rulenge white Stars,Mabawe FC,Kabanga FC,Ngara Stars,Walimu FC,Kumubuga FC na Murusagamba FC.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad