Awamu ya Pili ya Operesheni Kimbunga imeweza kukamata majambazi ya kutumiasilaha 67 na wahamiaji haramu 134. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, September 30, 2013

Awamu ya Pili ya Operesheni Kimbunga imeweza kukamata majambazi ya kutumiasilaha 67 na wahamiaji haramu 134.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIAWIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHITAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARIOPERESHENI KIMBUNGA AWAMU YA PILI YASHIKA KASI KATIKA MIKOA YAKAGERA, KIGOMA NA GEITA.

Awamu ya Pili ya Operesheni Kimbunga imeweza kukamata majambazi ya kutumiasilaha 67 na wahamiaji haramu 134 katika kipindi cha wiki moja tangu kuanzakwake Septemba 21hadi Septemba 27 mwaka huu katika mikoa ya Kagera, Kigomana Geita.


Silaha zilizokamatwa ni pamoja na bunduki aina ya SMG Moja, Pisto Moja naMagobole 17 pamoja na risasi 115 zikiwemo za bunduki aina ya SMG 102 na Risasiza Pisto 13.

Aidha, Magazine mbili zilikamatwa pamoja na Sare za Jeshi la Burundi.Wahamiaji haramu waliokamatwa wengi wao ni kutoka nchi za Burundi ambapo raiawake 114 walikamatwa wakiishi nchini kinyume na sheria wakati raia wa Rwanda 20walikamatwa katika kiindi hicho. 

Aidha, watu Watatu walikamatwa kwa tuhuma za kuhifadhi wahamiaji haramu nchinihuku Lita 271 za gongo , ngozi ya Mbwea, Bangi kilo Tatu na Makokoro 12vilikamatwa wakati wa operesheni Kimbunga awamu ya Pili ikiwa katika wiki yake yakwanza.

Wakati huo huo, Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera imejipanga kukabiliana na tatizola wahamiaji haramu ili kuhakikisha kuwa tatizo hilo linafikia mwisho wake na kuwapanafasi wananchi kufanya shughuli zao za kijamii na kimaendeleo bila ya hofu yakufanyiwa uhalifu na wahamiaji haramu.

Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Bi Dari Rwegasira amewaambia Maafisa Tarafa naWatendaji wa Kata aliokutana nao katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya yaKaragwe, mwishoni mwa wiki iiliyopita kuwa kuanzia sasa kila kiongozi, kuanziangazi ya Kiijiji/Mtaa, Kata, Tarafa na Wilaya, atawajibika kwa jinsi anavyoshughulikiakumaliza tatizo la wahamiaji haramu katika eneo lake.

Wilaya ya Karagwe ni moja ya wilaya zenye tatizo sugu la wahamiaji haramu ambaowanatuhumiwa kuwanyanyasa wananchi katika baadhi ya maeneo ya Wilaya hiyo,

kwa kuendesha vitendo vya wizi wa mifugo, kuvamia maeneo ya kilimo, na pia
kuchochea uhalifu wa unyang’anyi wa kutumia silaha na kusababisha mauaji.

Wahamiaji hao haramu wanashutumiwa kufanya baadhi ya maeneo ya Wilaya yaKaragwe yasipitike kwa urahisi, mojawapo ikiwa ni eneo la msitu wa Kimisi, ambapoeneo hili limekuwa na matukio mengi ya ujambazi wa kutumia silaha na wananchikuvamiwa na kuibiwa mali zao na hata wengine wakipoteza maisha katika matukiohayo.

Maazimio kadhaa yalitolewa katika kikao hicho kati ya Mkuu wa Wilaya ya Karagwena Watendaji Wakuu wa Wilaya hiyo, ikiwa ni pamoja na kuwa:
Viongozi kuanzia ngazi ya Kijiji/Kitongoji, Kata hadi Tarafa kutia saini mkatabawa kushughulikia wahamiaji haramu, majambazi wa kutumia silaha nawafadhili wao, mifugo haramu inayoingia nchini kutoka nchi jirani pamoja navitendo vyote vya uhalifu katika maeneo wanayoyaongoza.
Kiongozi yoyote wa Kijiji, Kata au Tarafa atakayeshindwa kushughulikiawahamiaji haramu walioko katika eneo lake atawajibishwa.
Wahamiaji wote haramu ambao bado wapo katika maeneo mbalimbali yawilaya hiyo wasakwe na kurejeshwa kwao mara moja.
Msako uanzishwe mara moja kuwasaka wahamiaji haramu wote ambaowamejificha katika maeneo ya misitu na ranchi za mifugo zilizoko katika wilayahiyo kwa kuvishirikisha vyombo vyote vya Utawala na vya Ulinzi na Usalamavilivyoko katika Wilaya hiyo.
Kila kijiji kiwe na takwimu sahihi za wageni waliopo katika maeneo yao.
Wahamiaji haramu wote wanaorejeshwa kwao wasipewe nafasi ya kurudi tenanchini na mwananchi yoyote atakayebainika kuwapokea au kuwasaidiakurejea atolewe taarifa haraka ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.
Vibali vyote vya Ukazi vilivyotolewa kwa wageni mbalimbali sasa vitakaguliwaupya ili kuhakiki uhalali wake.

Imeandaliwa na Timu ya Habari ya Operesheni Kimbunga Septemba30,2013

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad