Liverpool wameshika hatamu ya Ligi Kuu Uingereza baada kuifunga Bao 3-1 Crystal Palace huku Manchester City cha Bao 3-1. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, October 05, 2013

Liverpool wameshika hatamu ya Ligi Kuu Uingereza baada kuifunga Bao 3-1 Crystal Palace huku Manchester City cha Bao 3-1.

Kipigo cha Everton Uwanjani  Etihad  mikononi mwa Wenyeji Manchester City cha Bao 3-1, kimefuta rekodi ya Everton ya kuwa Timu pekee ambayo ilikuwa haijafungwa kwenye Ligi Kuu Uingereza Msimu huu na Ushindi huu umewafanya Man City wapande hadi Nafasi ya Pili wakiwa wamecheza Mechi moja zaidi na hivyo Mechi za baadae zinaweza kuwang’oa Nafasi hiyo.

Everton ndio walitangulia kufunga kwa Bao la Mchezaji wa Mkopo kutoka Chelsea, Romelu Lukaku na kudumu Dakika moja tu kwa City kusawazisha kwa Bao la Dakika ya 17 kuvitia Alvaro Negredo na Sergio Aguero kuipa City Bao la Pili kabla Haftaimu.
Timu ya Manchester City imemaliza rekodi ya Everton kutofungwa katika Ligi Kuu ya Uingereza baada ya leo hii (Octoba 05,2013) kuifunga mabao 3-1.

Contrasting fortunes: Joe Hart.
Vipigo vya Aston Villa na Bayern Munich viliwafanya City waingie kwa hasira leo na kipa wao 'kimeo' Joe Hart na kufanya kweli Uwanja wa Etihad Stadium.

Romelu Lukaku aliifungia Everton bao la kuongoza dakika ya 16, lakini Alvaro Negredo akasawazisha dakika moja baadaye na Sergio Aguero akafunga la pili kabla ya mapumziko.

Bao la tatu la City lilifungwa kufuatia Penati ya kilaini iliyotolewa baada Zabaleta kusukumwa huku Everton wakinyimwa Penati ya aina hiyo hiyo kufuatia kuangushwa Lukaku.


Aguero alipiga Penati hiyo iliyochezwa na Kipa Tim Howard na kugonga mwamba na Mpira kumbabatiza Kipa huyo na kutinga.

Nao Timu ya Liverpool wameshika hatamu ya Ligi Kuu Uingereza baada kuifunga Bao 3-1 Crystal Palace katika Mechi iliyochezwa Anfield.

Bao zote za Liverpool zilifungwa Kipindi cha Kwanza na Luis Suarez, Daniel Sturride na Penati ya Steven Gerrard iliyotolewa baada ya Raheem Sterling kuangushwa ndani ya boksi.

Bao la Crystal Palace lilifungwa katika Dakika ya 77 na Dwight Gayle.

RATIBA:-BPL: LIGI KUU ENGLAND 2013/2014.

Jumamosi 5 Oktoba,2013.

Manchester City  3-1  Everton

Cardiff City 1 -2 Newcastle United

Fulham 1 -0 Stoke City

Hull City 0 -0 Aston Villa

Liverpool 3 -1 Crystal Palace

19:30 Sunderland v Manchester United

Premier League

Table

TeamPPts

Jumapili 6 Oktoba,2013.

15:30 Norwich City v Chelsea

15:30 Southampton v Swansea City

18:00 West Bromwich Albion v Arsenal

18:00 Tottenham Hotspur v West Ham United

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad