VPL 2013/2014 :-Wekundu wa Msimbazi Simba wamepunguzwa kasi baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Maafande wa Ruvu Shooting ,Kesho ni Yanga SC na Mtibwa Sugar katika Uwanja wa taifa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, October 05, 2013

VPL 2013/2014 :-Wekundu wa Msimbazi Simba wamepunguzwa kasi baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Maafande wa Ruvu Shooting ,Kesho ni Yanga SC na Mtibwa Sugar katika Uwanja wa taifa.

Matokeo hayo, yanaifanya Simba SC
 itimize pointi 15 baada ya mechi saba
na kuendelea kushikilia usukani wa Ligi Kuu.
Ligi Kuu Soka ya Vodacom Tanzania Bara imeendelea leo(Octoba 05,2013) huku vinara Simba SC wakipunguzwa kasi kwa sare ya bao 1-1 na Ruvu Shooting  katika Uwanja wa Taifa, Mjini Dar es Salaam na Azam FC pia wakitoka sare ya bila kufungana na Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Simba SC ililazimika kusubiri hadi dakika ya 51 kupata bao la kusawazisha kwa penalti kupitia kwa Amisi Tambwe, kufuatia Betram Mombeki kuangushwa kwenye eneo la hatari, baada ya Ruvu Shooting kutangulia kufunga dakika ya nane kupitia kwa Said Dilunga.

Hata hivyo, wachezaji wa Ruvu Shooting walimzonga refa Mohamed Theophil wakipinga penalti hiyo, kabla ya kulainika na kukubali ipigwe- na Mrundi Tambwe akaenda kufunga bao lake la Nane ndani ya mechi saba katika msimu wake wa kwanza Simba SC.

Matokeo hayo, yanaifanya Simba SC itimize pointi 15 baada ya mechi saba na kuendelea kushikilia usukani wa Ligi Kuu.

Baadhi ya wachezaji wa Coastal Union.
Uwanja wa Mkwakwani, Tanga mechi ilikuwa kali, ilitawaliwa na vurugu za mashabiki tangu hata kabla mchezo haujaanza na matokeo kumalizika kwa sare ya bao 0 - 0.

Baada ya kucheza na Azam FC siku ya jumamosi  Octoba 05), Wagosi wa Kaya watakuwa wamebakisha mechi sita kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi kuu ambazo ni dhidi ya Ashanti United Octoba 13 siku ya Jumapili katika uwanja wa Chamazi  jijini Dar es Salaam.

Mechi nyingine ni dhidi ya Kagera Sugar (J2 Oct 19, Bukoba), Simba SC (J5 Oct 23, Tanga), Mtibwa Sugar (J1 Oct 26, Tanga), Mgambo JKT (J5 Oct 30, Tanga), mwisho watamalizia mzunguko wa kwanza katika Mkoa wa Pwani wakicheza dhidi ya JKT Ruvu Jumamosi Novemba 2.

Kikosi cha Timu ya Mbeya City wakiwa katika picha ya Pamoja katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha…magoli 2 ya timu hiyo yamefungwa na Paulo Nonga dakika ya 20 goli la kwanza na Peter Mapunda akiwa ameipatia Mbeya City Fc Goli la pili lililofungwa dakika ya 39.

Kikosi cha Timu ya Mbeya City wakiwa katika picha ya Pamoja katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha…na Goli la kwanza Lililo Fungwa na Expedito Kiduko dakika ya 35 ya mchezo huo.

MATOKEO /RATIBA LIGI KUU VODACOM  TANZANIA BARA 2013/2014.
Jumamosi Oktoba 05,2013.

Ruvu Shootings 1-1 Simba SC

JKT Ruvu 2-0 Kagera Sugar

Coastal Union 0-0 Azam FC

JKT Oljoro 1-2 Mbeya City


VPL-MSIMAMO 2013/2014.

NA
TIMU
P
W
D
L
GD
GF
POINTI
1
Simba SC
7
4
3
0
11
16
15
2
JKT Ruvu
7
4
0
3
4
8
12
3
Azam FC
7
2
5
0
3
9
11
4
Coastal Union
7
2
5
0
3
6
11
5
Mbeya City
7
2
5
0
2
8
11
6
Kagera Sugar
7
3
2
2
2
7
11
7
Ruvu Shooting
7
3
1
3
2
7
10
8
Yanga SC
6
2
3
1
4
11
9
9
Rhino Rangers
7
1
4
2
-1
7
7
10
Mtibwa Sugar
6
1
4
1
-1
5
7
11
JKT Oljoro
7
1
2
4
-3
4
5
12
Mgambo JKT
6
1
2
3
-8
2
5
13
Prisons FC
6
0
4
2
-6
3
4
14
Ashanti United
7
0
2
5
-11
4
2


Jumapili (Octoba 06,2013) Mabingwa watetezi Yanga watakuwa Nyumbani Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kucheza na Mtibwa Sugar.

Jumapili Oktoba 6,2013.

Yanga v Mtibwa Sugar

Mgambo JKT v Tanzania Prisons

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad