![]() |
|
Mabaki ya
jengo la Westgate lililoporomoka
baada ya
shambulizi la kigaidi jijini Nairobi,
Kenya.Picha
na Daily Mail.
|
Wiki moja
baada ya shambulizi la kigaidi kwenye jengo la Westgate jijini Nairobi, Kenya,
unyama wa kutisha uliofanywa na magaidi wa Al-Shabaab dhidi ya raia waliokuwa
wametekwa umebainika.
Taarifa
zilizochapishwa na gazeti la Daily Mail la uingereza zikiwakariri wanausalama
wa Kenya zinadai kuwa magaidi waliwatesa, kuwakata vidole, kuwanyofoa macho,
kuwahasi wanaume na kisha kuwaning’iniza darini.
Baadhi ya
mateka walinyofolewa kucha kwa koleo na maiti za watoto zilikutwa ndani ya
majokofu zikiwa na zimechomwa visu.
Askari
walieleza kuwa matukio hayo yalibainika muda mfupi baada ya kuingia kwenye
jengo hilo lililokuwa likishikiliwa na magaidi kwa siku tatu, na baadaye
kuporomoka kutokana na mashambulizi baina ya magaidi na majeshi ya Kenya.
Kwa mujibu
wa taarifa hizo, miili ya magaidi iliyopatikana ilikutwa imeungua na kubaki
majivu, tukio lililotafsiriwa kuwa ilikuwa njia ya kuficha utambulisho wao.
Inaelezwa
kuwa miili hiyo iliteketezwa na gaidi mmojawapo aliyebaki kwa ajili ya
usimamizi wa kufika utambulisho wao.
Hata hivyo
wapelelezi wa Kenya wanaoshirikiana na wenzao kutoka Shirika la Kijasusi la
Marekani (FBI) na Police wa Kimataifa wanaendelea kuchunguza mabaki ya jengo
hilo huku ikikadiriwa kuwa itachukua wiki moja kumaliza kazi hiyo.
![]() |
| Jengo la Westgate kabla ya Kushambuliwa. |
Idadi ya
vifo kuongezeka
Baada ya
vifuso vya jengo hilo kufukuliwa, idadi ya watu waliopoteza maisha kwenye
shambulio hilo imeelezwa inaweza kuongezeka kufikia 130 kutoka 61.
Hata hivyo,
hadi jana takwimu zilizotolewa na serikali ya nchi hiyo, zilikuwa zinaonyesha
kuwa watu waliopoteza maisha walikuwa 67, saba kati yao wakiwa ni wanausalama.
Hata hivyo,
Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya, limesema kuwa watu 63 walikuwa
hawajulikani walipo.
Kama watu
hao watakuwa chini ya kifusi ambacho tayari kimeanza kufukuliwa, uwezekano wa
vifo kuongezeka na kufikia 130 ni mkubwa.
Kwa mujibu
wa Gazeti la Daily Mail la Uingereza, idadi hiyo ikiongezeka itafanya pia raia
wa Uingereza waliopoteza maisha kufika 10 kutoka sita waliothibitishwa kufa
hadi sasa.
Al Shabaab
wametoa taarifa kupitia mtandao wa Twitter wakisema katika tukio hilo waliuawa
watu 137.
![]() |
|
Waziri wa
usalama wa ndani wa Kenya
Bw.Joseph
Ole Lenk.
|
Bunge
kuwahoji wanausalama
Viongozi
wakuu wa ujasusi nchini Kenya wametakiwa kufika mbele ya Kamati ya Ulinzi ya
Bunge la nchi hiyo ili kutoa maelezo kuhusu shambulizi la kigaidi lililotokea
kwenye jengo la Westgate.
Kamati ya
bunge inataka maofisa wanaohusika na masuala ya usalama wafike mbele ya tume
hiyo Jumatatu ili waweze kuwajibishwa kutokana na tukio hilo lililo sababisha
vifo vya watu 67 na wengine 175 kujeruhiwa.
Uhamiaji
Tanzania yakanusha
Wakati
kukiwa na taarifa kuwa mwanamke anayedaiwa kupanga mashambulizi hayo, Samantha
Lewthwaite alipita katika mpaka wa Namanga hapa nchini, Msemaji Mkuu wa Idara
ya Uhamiaji, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Abbas Irovya amekanusha taarifa hizo.
Irovya
amesema hakuna kumbukumbu za mwanamke huyo katika mipaka iliyotajwa kwa kuwa
ina mitambo ya kisasa ya kuhifadhi taarifa na pia kugundua paspoti bandia.
“Huyu
mwanamke hajawahi kutumia mipaka hiyo kwa kuwa hakuna kumbukumbu zake, kama
angepita tungeziona, na hata hiyo pasipoti yake ni bandia kwa mujibu wa
Serikali ya Afrika Kusini, hivyo kwa vyovyote angekamatwa tu katika mipaka
hiyo,” anasema Irovya.
Taarifa za
Shirika la Kimataifa la Polisi (Interpol) zinasema mwanamke huyo aliwahi kupita
Tanzania mwaka 2011 akitumia mipaka ya Lunga Lunga na Namanga mkoani Arusha
akitumia jina la Webb Natalie Faye.
Chanzo:Mwananchi.








No comments:
Post a Comment