‘Wahamiaji walioolewa na Watanzania wanaruhusiwa kubaki Nchini’ - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, September 10, 2013

‘Wahamiaji walioolewa na Watanzania wanaruhusiwa kubaki Nchini’

Serikali ya Tanzania imesema Raia wanaoishi nchini Kinyume cha Sheria ,walioolewa na Watanzania wanaruhusiwa kubaki nchini, hawalazimiki kuvunja ndoa zao ingawa wanatakiwa kupata kibali maalumu kutoka Idara ya Uhamiaji.

Akizungumza mjini Bukoba jana (Septemba 09,2013), Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Mstaafu Fabian Massawe, alisema wahamiaji hao walioolewa wanatakiwa kwenda Idara ya Uhamiaji kupata hati hizo.

Hatupendi kuachanisha familia zilizoishi kwa zaidi ya miaka miwili mfululizo, wanatakiwa kwenda uhamiaji kuhalalishwa na baadaye ikigundulika hana tatizo anaweza kupewa uraia,” alisema Kanali Massawe.

Pia, alisema kwa mujibu wa sheria, mhusika atapewa kibali alichokiita ‘Independence Pass’ kitakachomwezesha kuendelea kuishi  nchini na kwamba, kinyume chake itakuwa ni kuvunja haki za binadamu.

Kanali Mstaafu Fabian Massawe.
Hata hivyo, Kanali Massawe alibainisha kuwa lazima zoezi la kuondoa wahamiaji lifanyike, kwani walioondoka kwa hiari ni 11,601 na waliokadiriwa kuondoka ni kati ya 52,000 na 53,000, hivyo idadi kubwa bado wanaishi nchini.

Akizungumzia zoezi la kurudisha Raia wanaoishi Nchini kinyume che Sheria na utaratibu wa Idara ya Uhamiaji lililoanza rasmi Septemba 6, mikoa ya Kagera, Geita na Kigoma, Mkuu Msaidizi wa Operesheni hiyo, Simon Sirro, alisema tayari wamewakamata  1,851.

Pia, Sirro alisema ng’ombe 1,765, sare za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na bunduki saba vimekamatwa  na kwamba, wahamiaji  wanaokamatwa wanarudishwa kwa mujibu wa sheria kwa kuzingatia haki za binadamu.


Na Phinias Bashaya:- Mwananchi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad