Mabingwa wa wilaya ya Ngara Murusagamba FC yaiondosha Kabanga FC kuwania Brayan Cup 2013. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, September 08, 2013

Mabingwa wa wilaya ya Ngara Murusagamba FC yaiondosha Kabanga FC kuwania Brayan Cup 2013.


Kikosi cha Wachezaji wa Murusagamba FC wakiwa katika mapunziko ya kipindi cha kwanza cha mchezo wao Leo Jumapili (Septemba 08.2013) waliposhuka katika uwanja wa Kokoto kumenyana na Timu ya Kabanga FC  na Katika mchezo huo ,timu ya Murusagamba FC  imetinga  hatua ya Fainali ya Brayan Cup  kwa kuitwanga Kabanga FC mabao    2-1.


Bi.Rehema Ramadhani ambaye ni Diwani Viti Maalumu ,tarafa ya Murusagamba akifatilia kila tukio la mchezo kwenye uwanja wa Kokoto Mjini Ngara kati ya Timu yake ya  Murusagamba  waliposhuka kumenyana na Timu ya Kabanga FC  na Murusagamba FC  kuitwanga Kabanga FC mabao 2-1.

Baadhi ya Viongozi wa Tarafa ya  Murusagamba wilayani Ngara mkoani Kagera wakiwa wamefatana na timu yao ya Murusagamba FC wakiwa  uwanja wa Kokoto Mjini Ngara  kuutazama mchezo kati ya Timu  ya  Murusagamba  waliposhuka kumenyana na Timu ya Kabanga FC  na Murusagamba FC  kuitwanga Kabanga FC mabao 2-1.

Timu hizo zikimenyana katika uwanja wa wilaya ya Ngara  wa Kokoto ambao hauna kiwango kizuri cha kuchezewa mechi ambapo Murusagamba FC wamefanikiwa kutinga Fainali ya kuwania Brayan Cup.



Muonekano wa Baadhi ya wachezaji wa timu ya kabanga FC ya Mjini Kabanga wilayani Ngara ,mkoani Kagera wakiwa  katika mapumziko ya kipindi cha kwanza katika mchezo wao dhidi ya Mabingwa wa Soka wilaya ya Ngara, Timu ya Murusagamba FC wakati wa mchezo wao kwenye uwanja wa Kokoto kuwania Brayan CUP 2013.


Muonekano wa Mashabiki wakifatilia mchezo  kati ya Timu  ya  Murusagamba FC waliposhuka kumenyana na Timu ya Kabanga FC  na Murusagamba FC  kuitwanga Kabanga FC mabao 2-1.

Hiki ni Kikosi cha timu ya soka ya Wanawake ya Runazi toka wilayani Biharamulo mkoani Kagera ambayo leo Jumapili(Septemba 08,2013) imesafiri kuja hapa wilayani Ngara kucheza na wenzao wa Ngara na kufanikiwa kuwafunga bao 1-0 katika mchezo wa kirafiki wa kiujirani mwema baina ya timu hizo za soka la wanawake,mchezo ukichezwa katika uwanja wa Posta ya Zamani hapa mjini Ngara.

Bi.Niniani Bakari mratibu wa  soka la Wanawake wilayani Ngara mkoani Kagera na pia Diwani wa Viti Maalumu tarafa ya Kanazi  ,ambaye leo alishuhudia timu yake ya Ngara ikifungwa bao 1-0 na Runazi .

Afisa Michezo wa wilayani Biharamulo  mwenye kofia Dioniz Magezi akiwa na Mwl Adolf Gisuka wakiwa na mchezaji wa soka la kike  leo(Septemba 08,2013) kwenye uwanja wa Posta ya zamani ,Mjini Ngara.
Mashindano ya kuwania Kombe la Brayan au BRAYAN CUP 2013 ,inayoshirikisha timu  toka wilayani Ngara mkoani Kagera  na Ijumaa ,Jumamosi(Septemba 07,2013) na Jumapili (Septemba 08,2013) michezo ya hatua ya Robo fainali ilichezwa katika Uwanja wa Kokoto Mjini Ngara.

 Siku ya Ijumaa(Septemba 05,2013) Timu ya Walimu FC ilifanikiwa kuingia hatua ya Mwisho ya Fainali kwa kuwaondosha  Rulenge White Stars kwa kuwafunga magoli 2-1 kwa magoli ya Mwl.Severin John na Moses John.

Jumamosi(Septemba 07,2013) Ngara Stars wakaondoshwa na Vijana wa Boda-Rusumo FC kwa kuzabwa bao 1-0 katika mchezo ulienda dakika 120 baada ya dakika 90 timu hizo kutoshana nguvu ya bila kufungana.

Leo Jumapili (Septemba 08.2013) Mabingwa wa soka wa wilaya Murusagamba FC wameshuka katika uwanja huo wa Kokoto kumenyana na Timu ya Kabanga FC  na Katika mchezo huo ,timu ya Murusagamba FC  imetinga  hatua ya Fainali ya Brayan Cup  kwa kuitwanga Kabanga FC mabao 2-1, yaliyofungwa na Gilbaert Gozibert  na Egason Fredrick huku Kabanga  FC bao lao la  kufutia machozi likifungwa na Yasiri Jumanne.


Kombe hilo sasa limemaliza michezo ya hatua ya Robo Fainali na timu zilizofanikiwa kusonga mbele ni Walimu FC,Rusumo FC na Murusagamba FC ambao kwa mujibu wa kanuni timu hizo zitacheza mtindo wa Ligi(Pointi) ili kumpata Bingwa wa Brayan Cup 2013 ambaye mshindi wa kwanza ataondoka na zawadi ya shilingi 300,000. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad