VPL 2013/2014:-Bingwa Mtetezi Yanga SC yapoteza mchezo wake wa kwanza tangu mwisho mwa mwaka Jana dhidi ya Azam FC baada ya kufungwa mabao 3-2. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, September 22, 2013

VPL 2013/2014:-Bingwa Mtetezi Yanga SC yapoteza mchezo wake wa kwanza tangu mwisho mwa mwaka Jana dhidi ya Azam FC baada ya kufungwa mabao 3-2.



Klabu ya  Azam FC imefanikiwa kufuta uteja kwa Mabingwa wtetezi wa Ligi kuu Vodacom Tanzania bara ,Yanga SC baada ya leo(Septemba 22,2013) kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Aidha goli  la Dakika ya 90 la  Mchezaji   kinda aiyepandishwa kutoka kikosi cha pili,Joseph Kimwaga limewapa ushindi  huo Azam FC wa Bao 3-2.


Azam FC walitangulia kufunga kwa Bao la Dakika ya Kwanza tu  Mfungaji akiwa John Bocco na Bao hilo kudumu hadi Mapumziko.

Kipindi cha Pili Yanga waliibuka na kusawazisha kwa Bao la Kavumbagu na kwenda mbele kwa Bao 2-1 kwa Bao la Hamis Kiiza.

Azam FC walisawazisha kwa Penati iliyopigwa na Kipre Tchetche baada Kevin Yondani kushika Mpira na Gemu kuwa 2-2.

 

Kwa matokeo hayo sasa yanaifanya Yanga SC kuwa imepoteza mchezo wake wa kwanza katika Ligi Kuu ya Vodacom tangu mwisho mwa mwaka jana dhidi ya timu ya Azam FC baada ya kufungwa mabao 3-2 katika mchezo uliofanyika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Huu unakuwa ushindi wa pili kwa Azam msimu huu ndani ya mechi tano na sasa inafikisha pointi tisa, wakati kwa Yanga SC hiki ni kipigo cha kwanza ndani ya mechi tano, wakiwa pia wametoa sare tatu na kushinda mechi moja, hivyo wanabaki na pointi zao sita.


Katika mechi nyingine za ligi hiyo kuu soka Vodacom Tanzania bara, JKT Ruvu ilifungwa 1-0 na JKT Oljoro Uwanja wa Azam Complex, bao pekee la Paul Malipesa dakika ya 79, Ruvu Shooting ililala 1-0 mbele ya Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, bao pekee la Haruna Moshi ‘Boban’ dakika ya 82.

LIGI KUU VODACOM 2013/2014 MATOKEO.


Jumamosi Septemba 21,2013.


Mgambo JKT 1 – 1 Rhino Rangers



Tanzania Prisons 1 – 1  Mtibwa Sugar



Kagera Sugar 3 – 0 Ashanti United



Simba SC  2 – 2 Mbeya City 


Jumapili Septemba 22,2013.

Azam FC 3 -2  Yanga  SC



Coastal Union 1 – 0 Ruvu Shooting



JKT Ruvu 0 – 1 JKT Oljoro 


VPL-MSIMAMO:-2013/2014.


NA TIMU P W D L GD GF POINTI
1 Simba SC 5 3 2 0 9 13 11
2 JKT Ruvu 5 3 0 2 4 6 9
3 Azam FC 5 2 3 0 3 8 9
4 Ruvu Shooting 5 3 0 2 3 6 9
5 Coastal Union 5 2 3 0 3 5 9
6 Kagera Sugar 5 2 2 1 3 6 8
7 Mbeya City 5 1 4 0 1 6 7
8 Yanga SC 5 1 3 1 3 10 6
9 Mtibwa Sugar 5 1 3 1 -1 4 6
10 Rhino Rangers 5 0 4 1 -2 5 4
11 JKT Oljoro 5 1 1 3 -2 3 4
12 Mgambo JKT 5 1 1 3 -8 2 4
13 Prisons FC 5 0 3 2 -6 2 3
14 Ashanti United 5 0 1 4 -9 2 1


**MSIMAMO TOKA TFF

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad