VPL 2013/14:- Simba SC yaburuza 6-0, Yanga SC na Azam FC zabanywa mbavu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, September 18, 2013

VPL 2013/14:- Simba SC yaburuza 6-0, Yanga SC na Azam FC zabanywa mbavu.




Kikosi cha Young Africans kilichoanza katika mchezo dhidi ya Prions FC :- Young Africans imetoka sare ya bao 1-1 dhidi ya wenyeji timu ya Prisons FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliochezwa jioni ya leo(Septemba 18,2013)  katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Wekundu wa msimbazi Simba SC imeonyesha ni tishio msimu huu baada tya kushinda mabao 6-0 dhidi ya Mgambo JKT katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, huku mshambuliaji Mrundi, Amisi Tambwe akifunga mabao manne peke yake.

Mabao mengine ya Simba leo(Septemba 18,2013) yamefungwa na kinda mzalendo, Haroun Athumani Chanongo, huku wapinzani wao wa jadi, Yanga SC wakilazimishwa sare ya 1-1 na Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

Matokeo hayo yanaipandisha kileleni Simba SC baada ya kufikisha pointi 10 kutokana na mechi nne, huku Yanga SC na Azam FC zinaendelea kusuasua kwa pointi zao sita kila mmoja baada ya mechi nne.

Tambwe aliyetokea Vital’O ya Burundi alifunga mabao manne leo katika dakika za nne, 41, 44 na 76 kwa penalti, baada ya beki Bashiru Chanache wa Mgambo kuunawa mpira kwenye eneo la hatari, wakati Haroun Chanongo alifunga mawili pia dakika ya 32 na 64.

Kwa ujumla Simba SC iliwapa raha mashabiki wake leo kwa soka safi na ushindi mnono.
 

Kikosi cha Coastal Uinion kilichoanza leo.
Huko Mbeya; Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, Jerry Tegete alitangulia kuifungia Yanga SC dakika ya 37 akiunganisha krosi maridadi ya winga Simon Msuva kabla ya Michael Peter kuisawazishia Prisons dakika ya 77 akiunganisha krosi ya Omega Seme anayecheza kwa mkopo kutoka Jangwani. 

Yanga SC ilicheza vizuri zaidi kipindi cha kwanza na kupoteza nafasi mbili nzuri za kufunga mabao zaidi dakika ya tatu, Didier Kavumbangu alipowababatiza mabeki shuti kali baada ya kupokea krosi ya Simon Msuva na Jerry Tegete dakika ya saba aliwatoka vizuri mabeki wa Prisons, lakini akapiga nje.

Yanga walionekana kupigana zaidi kusaka bao la ushindi, lakini Prisons walisimama imara kuzuia na kushambulia pia na dakika ya 87 almanusra Prisons wapate bao la pili baada ya Ibrahim Isihaka kupiga kichwa juu kidogo ya lango kufuatia krosi ya Julius Kwanga.   

Kule Uwanja Chamazi:- Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, Kipre Tchetche alitangulia kuifungia Azam dakika ya 21, kabla ya Anthony Matangalu kuisawazishia Ashanti United dakika ya 79.

Katika mchezo huo, Azam ilimalioza pungufu baada ya Aggrey Morris kutolewa nje kwa kadi nyekundu.

Uwanja wa Mabatini, Mlandizi Mkoani Pwani:-  Ruvu Shooting iliichapa 1-0 JKT Ruvu, bao pekee la Cossmas lewis dakika ya 36.

Uwanja wa Kaitaba, Bukoba:- Wenyeji Kagera Sugar waliifunga JKT Oljoro 2-1.  Mabao ya Kagera yalifungwa na Godfrey Wambura dakika ya 25 na Maregesi Mwangwa dakika ya 90, wakati la Oljoro lilifungwa na Shaibu Nayopa dakika ya 35.


Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro:- wenyeji Mtibwa Sugar walilazimishwa sare ya bila kufungana na Mbeya City, wakati Coastal Union ililazimishwa sare ya 1-1 na Rhino Rangers ya Tabora.

Mkenya Jerry Santo aliinusuru Coastal kuzama kwa bao la penalti dakika ya 81, kufuatia Salum Majjid kutangulia kuifungia Rhino dakika ya 26.  

RATIBA:
Jumamosi Septemba 21,2013.

Mgambo JKT v Rhino Rangers

Tanzania Prisons v Mtibwa Sugar

JKT Ruvu v JKT Oljoro

Simba v Mbeya City

Azam FC v Yanga

Kagera Sugar v Ashanti United

Coastal Union v Ruvu Shooting


VPL-MSIMAMO:

NA
TIMU
P
W
D
L
GD
GF
POINTI
1
Simba SC
4
3
1
0
9
11
10
2
JKT Ruvu
4
3
0
1
5
6
9
3
Ruvu Shooting
4
3
0
1
4
6
9
4
Yanga SC
4
1
3
0
4
8
6
5
Azam FC
4
1
3
0
2
5
6
6
Coastal Union
4
1
3
0
2
4
6
7
Mbeya City
4
1
3
0
1
4
6
8
Mtibwa Sugar
4
1
2
1
-1
3
5
9
Kagera Sugar
4
0
3
1
-1
2
3
10
Rhino Rangers
4
0
3
1
-2
4
3
11
Mgambo JKT
4
1
0
3
-8
1
3
12
JKT Oljoro
4
0
2
2
-3
2
2
13
Prisons FC
4
0
2
2
-6
1
2
14
Ashanti UTD
4
0
1
3
-6
2
1

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad