Mradi wa Umeme wa maporomoko ya Maji ya Mto Rusumo Mkoani Kagera wasainiwa ili kuanza kujengwa mwaka 2015. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, September 18, 2013

Mradi wa Umeme wa maporomoko ya Maji ya Mto Rusumo Mkoani Kagera wasainiwa ili kuanza kujengwa mwaka 2015.


Mawaziri  wa Nishati ya Umeme kutoka nchi za Tanzania ,Rwanda na Burundi katika picha ya pamoja na wafadhili wa  Benki ya Dunia(WB ) na  Benki ya Maendeleo ya Africa (ADB) ambao wameshiriki majadiliano ya kusainiwa kwa mradi wa ujenzi wa umeme katika maporomoko ya maji ya   mto Rusumo  ulioko mpakani mwa nchi za Tanzania na Rwanda (Septemba 17,2013) mjini Bukoba.




Mawaziri watatu kutoka Tanzania Rwanda na Burundi wametiliana saini ya kuanza kutekeleza mradi wa uzalishaji umeme ulioko katika maporomoko ya Rusumo mpakani mwa Tanzania na Rwanda.

Waziri wa nishati na madini wa Tanzania Profesa Sospita Muhongo amesema hayo septemba 12,mwaka huu   katika mkutano wa sita wa wataalamu wa mradi huo  na mawaziri wa nchi zao uliofanyika katika manispaa ya Bukoba mkoani Kagera.

Profesa Muhongo amesema kuwa  wataalamu wa mradi huo  pamoja na wafadhili wa  wamejadiliana na kufikia makubaliano ya kuanza kuujenga mwaka 2015 na kuukamilisha mwaka 2018  kwani  ulioanza kufanyiwa utafiti tangu mwaka 1974.

Aidha Profesa Muhongo amesema katika ujenzi wa mradi huo wa  megawati 80   kila nchi itapata megawati 27  na mradi huo kila nchi itakuwa na usimamizi wa 30% ambapo asilimia nyinginezo zitawekezwa katika mto Nile.

Katika Hatua nyingine Profesa Muhongo amesema kuwa Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) imekubali kutoa shilingi milioni 870 kwa ajili ya kupeleka umeme kutoka mjini Ngara hadi Rusumo kwa wananchi na taasisi zake.

Ameongeza kuwa  watendaji wa shirika la umeme nchini TANESCO kanda ya ziwa hawana budi kufanya kazi kwa ushirikiano  ili kuhakikisha wanatoa huduma kwa wananchi kwa kuwapatia nishati ya umeme kwa wakati.

Watendaji wa wizara yangu  watumie  uzalendo katika kutekeleza masuala ya kitaifa katika mradi huu kwa  kuboresha maisha ya  wananchi kuliko kuhudhuria mikutano na  kutelekeza maazimio wanayokubaliana”. Akiongeza  kuwa “Serikali imedhamilia kusambaza umeme katika maeneo ya  vijijini katika halmashauri za wilaya  kwa  30% ifikapo mwaka 2015 ambapo na bajeti ya wizara yangu  mwaka huu  imeongezeka kutoka Bil 642 hadi Tilioni 1.4”.Alisema Muhongo.

Hata hivyo waziri wa nishati na madini wa Tanzania Profesa Sospita Muhongo ametoa rai kwa wazabuni ,wakandarasi na wataalamuwa mradi huo  kutumia uzalendo  kwa kuepuka mianya ya Rushwa na kuujenga chini ya viwango na kwamba atawachukulia hatua watakaofanya ubadhilifu.

Kwa upande wake waziri wa miundombinu wa nchini Rwanda profesa Silas Rwakabamba  amewashauri wananchi  wa nchi tatu zenye mradi huo   kutumia fursa zitakazojitokeza katika mradi wa uzalishaji umeme wa rusumo ili kuinua maisha yao kiuchumi.

Profesa  Rwakabamba amesema umeme huo utanufaisha wananchi zaidi ya nchi  tatu zilizolengwa kwa kujumuisha upatikanaji wa nafasi za ajira na kukuza kipato cha kiuchumi katika sekta mbalimbali.

Amesema katika utoaji wa ajira kwa wataalamu wa mradi huo  mawaziri wamekubaliana kuhakikisha zinatolewa fursa kwa nchi zote husika  ili kuhakikisha manufaa yanapatikana  bila kuwepo upendeleo wala hujuma yoyote.

Picha/Habari Na: Shaaban Ndyamukama.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad