Taswira ya Wanafunzi kutoka Shule 4 za Msingi wilayani Ngara Mkoani Kagera walivyoshiriki Bonanza la siku moja la Michezo la Jambo Bukoba. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, September 20, 2013

Taswira ya Wanafunzi kutoka Shule 4 za Msingi wilayani Ngara Mkoani Kagera walivyoshiriki Bonanza la siku moja la Michezo la Jambo Bukoba.


Wanafunzi  wapatao 107 kutoka  shule za Msingi za Buhororo,Rulenge,Munjebwe na Mayenzi wilayani Ngara Mkoani Kagera wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa Mashindano ya Bonanza la siku moja la Michezo mbalimbali Ngazi ya wilaya ya Ngara lililoandaliwa na Idara ya Elimu shule za Msingi kwa ufadhili wa shirika la Jambo Bukoba na kufanyika Septemba 20,2013 katika viwanja vya shule ya Msingi Buhororo.





Bonaza hilo lilifunguliwa na Kufungwa na Afisa Elimu Idara ya Msingi wilayani Ngara Bw.Simon Mumbee ambapo pamoja na mambo mengine alikabidhiwa zawadi ya Mpira wenye Maandishi ya Mdhamini wa Jambo Bukoba (Bayern Munich) na Ms.Sandra Kagerer kutoka Ujerumani kwa Niaba ya Jambo Bukoba mkoa wa Kagera.


 Afisa Elimu Idara ya Msingi wilayani Ngara Bw.Simon Mumbee akionesha zawadi ya Mpira aliyokabidhiwa na Jambo Bukoba mkoa wa Kagera na pembeni yake ni Afisa Michezo wilaya ya Ngara Saidi Salumu(track suit ya blue) na Mratibu Elimu Kata ya Kibimba.



Baadhi ya wanafunzi wa shule za Msingi za Buhororo,Rulenge,Munjebwe na Mayenzi wilayani Ngara Mkoani Kagera  wakiendelea na  michezo ya kuunda maumbo ya aina mbalimbali kwa kutumia kamba wakati wa Mashindano ya Bonanza la siku moja la Michezo mbalimbali Ngazi ya wilaya ya Ngara lililoandaliwa kwa ufadhili wa shirika la Jambo Bukoba na kufanyika Septemba 20,2013 katika viwanja vya shule ya Msingi Buhororo.



Afisa Elimu Idara ya Msingi wilayani Ngara Bw.Simon Mumbee akifungua Bonanza hilo la Jambo Bukoba kwa kuwataka washiriki kushiriki kwa ushindani pamoja na kulishukuru shirika la Jambo Bukoba kwa Kutoa Elimu na Kuibua vipaji pamoja na Kuviendeleza kupitia michezo kwa shule za msingi huku pembeni yake ni Mratibu wa Michezo toka Shirika la Jambo Bukoba mkoa wa Kagera Bw.Gonzaga Steven na Afisa Michezo wilaya ya Ngara Saidi Salumu.









Muonekano wa Wanafunzi wa shule ya msingi Buhororo wilayani Ngara mkoani Kagera wakiwa katika mashindano ya Bonanza dhidi ya wenzao kutoka Shule za Msingi Rulenge ,Munjebwe na Mayenzi wilayani humo ,Bonanza hilio liliandaliwa na  Idara ya Elimu shule za Msingi kwa ufadhili wa Shirika la Jambo Bukoba.



Wanafunzi  wapatao 107 kutoka  shule za Msingi za Buhororo,Rulenge,Munjebwe na Mayenzi wilayani Ngara Mkoani Kagera wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa Mashindano ya Bonanza la siku moja la Michezo mbalimbali Ngazi ya wilaya ya Ngara lililoandaliwa kwa ufadhili wa shirika la Jambo Bukoba na kufanyika Septemba 20,2013 katika viwanja vya shule ya Msingi Buhororo.


Bonanza hilo kwa Mujibu wa Afisa Elimu Idara ya Msingi wilayani Ngara Bw.Simon Mumbee amebainisha kuwa ni muendelezo wa michezo ambayoimekuwa ikifanyika toka mwaka jana ambapo kwa wilaya ya Ngara Mkoani Kagera timu 4 zilishiriki na kutoa Bingwa wake shule ya Msingi Rulenge ambayo ilienda kushiriki Bonanza la Jambo Bukoba ngazi ya Mkoa wa Kagera.

Michezo iliyochezwa ni pamoja na Kunyang’anyana mpira,Mchezo wa Aljebra,Mchezo wa partner football na Ten Pass.

Aidha Mratibu wa Michezo toka Shirika la Jambo Bukoba mkoa wa Kagera Bw.Gonzaga Steven amesema Bingwa wa Bonanza hilo atakayepatikana ataiwakilisha Wilaya ya Ngara katika Bonanza kama hilo Ngazi ya Mkoa wa Kagera hapo Mwakani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad