![]() |
Ujumbe kwa
kocha: Shabiki la Chelsea akipeleka ujumbe kwa kocha Mourinho kwamba Juan Mata
anastahili kucheza na si kukaa benchi.
|
![]() |
Oscar alitangulia kuwafungia The Blues dakika ya 45, lakini Salah
akasawazisha dakika ya 71, kabla ya Streller kufunga la ushindi dakika ya 82
Uwanja wa Stamford Bridge.
|
![]() |
Wachezaji Gary
Cahill, Oscar na John Obi Mikel wakionekana wanyonge wakati Basle wanashangilia
ushindi wao Stamford Bridge.
|
![]() |
Marco
Streller (wa pili kushoto) akiifungia bao la ushindi Basle jana (Septemba
18,2013) katika uwanja wa Stamford Bridge katika Mashindano ya UEFA 2013/2014.
|
![]() |
Streller
(katikati kushoto) akishangilia na mfungaji mwenzake Mohamed Salah.
|
![]() |
Nahodha
wa klabu, John Terry alisugua benchi.
|
![]() |
Aaron Ramsey
amefunga bao la sita msimu huu akiwa na Arsenal na hapa dakika ya 83 akiwapa
ushindi wa 2-1 dhidi ya wenyeji Marseille Uwanja wa Velodrome, Ufaransa.
|
![]() |
Arsenal
walifikiri walistahili kupewa penalti baada ya buti hili alilopigwa Per
Mertesacker.
|
![]() |
Rekodi ya
klabu: Arsenal imetweet mechi zake 10 ilizoshinda ugenini
|
![]() |
Muargentina
huyo Messi akifunga bao
lake la pili katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Ajax katika mchezo wa Kundi H wa
Ligi ya Mabingwa Ulaya, Uwanja wa Nou Camp.
|
![]() |
Wachezaji wa
AC Milan wakiwa wameweka ukutawakati beki wa kati wa Celtic, Charlie Mulgrew
akipiga mpira wa adhabu.
|
![]() |
Sulley
Muntari wa Milan akishangilia baada ya kufunga bao la pili zikiwa zimebaki dakika
tano.
|
![]() |
Mchezaji Phillipe
Mexes akimrukia Cristian Zapata baada ya Mcolombia kufunga kwa AC Milan iliichapa Celtic 2-0.
|
Sehemu ya
pili ya mzunguko wa kwanza wa hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa
barani ulaya imeendelea usiku wa jana (Septemba 18,2013) kwa michezo nane iliyopigwa kwenye miji
mikuu ya soka barani humo .
Kwenye
uwanja wa Nou Camp Fc Barcelona waliwafunga Ajax Amsterdam 4-1 huku Lioneln
Messi akiwa nyota wa mchezo baada ya kumjibu Cristiano Ronaldo kwa kufunga
mabao matatu pekee yake . Bao lingine la mchezo huo lilifungwa na beki Gerrard
Pique .
Jijini Milan
kwenye uwanja wa Giuseppe De Meazza Ac Milan walipata ushindi wa tabu
wakiwafunga Glasgow Celtic 2-0 . Wafungaji wa Milan kwenye mchezo huo walikuwa
Sulley Muntari na Cristian Zappata.
Katika
matokeo yaliyoshangaza wengi usiku wa jana (Jumatano) (Septemba 18,2013) mabingwa wa zamani wa
amshindano haya Chelsea The Blues walipoteza mchezo wao dhidi ya Fc Basle tena
kwenye uwanja wao wa nyumbani Stamford Bridge .
Basle walishinda kwa mabao
mawili kwa moja wafungaji wakiwa Marco Streller na Mohamed Salah huku Chelsea
wakifunga kupitia kwa Oscar.
Arsenal
waliendeleza mwanzo mzuri kwa timu za England kwenye msimu huu wa ligi ya
mabingwa baada ya kuwafunga Olympique Marseille kwa mabao mawili kwa moja .
Mabo ya
Arsenal yalifungwa na Theo Walcott na Aaron Ramsey huku Marseile wakifunga
kupitia kwa Jordan Ayew ambaye alifunga kwa mkwaju wa penati.
Mechi
iliyokuwa inatazamiwa na wengi kuwa mechi ngumu pengine kuliko mechi zote za
jana iliwakutanisha washindi wa pili wa ligi za Italia na Bundesliga Napoli na
Borrusia Dortmund .
Katika
mchezo huo uliopigwa huko Italia Napoli walishinda kwa mabao mawili kwa moja.
Wafungaji wa Napoli walikuwa Gonzalo Higuain na Lorenzo Insigne huku Camilo
Zuniga wa Napoli akijifunga mwenyewe kuipa Dortmund bao pekee lao mchezo huo .
Timu
nyingine toka Hispania Atletico Madrid ilishinda mchezo wao dhidi ya Zenith St
Petesburg kwa matokeo ya 3-1 huku Schalke 04 nao wakishinda mchezo wao dhidi ya
Steua Bucharest kwa 3-0 . Nao Fc Porto waliwafunga Austria Wien 1-0.
Matokeo ya
UEFA Champions League Septemba 18,2013.
Fc Barcelona
4-0 Ajax Amsterdam.
AC Milan 2-0
Glasgow Celtic .
Napoli 2-1
Borrusia Dortmund.
Marseile 1-2
Arsenal.
Chelsea 1-2
FC Basle.
Atletico
Madrid 3-1 Zenith St Petersburg.
Austria
Vienna 0-1 Fc Porto.
Schalke 04
3-0 Steua Buchares
Mechi zifuatazo ni za Hatua ya Pili ya Makundi UEFA 2013/2014:-Jumanne 1
Oktoba 2013.
FC Basel
1893 v FC Schalke 04
FC Steaua
BucureÅŸti v Chelsea FC
Borussia
Dortmund v Olympique de Marseille
Arsenal FC v
SSC Napoli
Football
Club Zenit v FK Austria Wien
FC Porto
Club v Atlético de Madrid
AFC Ajax v
AC Milan
Celtic FC v
FC Barcelona
Jumatano 2
Oktoba 2013.
FC Shakhtar
Donetsk v Manchester United FC
Bayer 04
Leverkusen v Real Sociedad de Fútbol
Juventus v
Galatasaray A.Åž.
Real Madrid
CF FC København
Paris
Saint-Germain v SL Benfica
RSC
Anderlecht v Olympiacos FC
Manchester
City FC v FC Bayern München
PFC CSKA
Moskva v FC Viktoria Plzeň






















No comments:
Post a Comment