Seikali ya kijiji cha Kasulo wilayani Ngara mkoani Kagera yakanusha Mauaji kutokea Kijijini humo. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, September 27, 2013

Seikali ya kijiji cha Kasulo wilayani Ngara mkoani Kagera yakanusha Mauaji kutokea Kijijini humo.


Mkuu wa wilaya ya Ngara mkoani Kagera Bw. Costantine Kanyasu akiwa porini  na kamati ya ulinzi na usalama kuangalia sehemu yalikofanyikia mauaji eneo la Ngoma kijiji cha Kasulo wilayani Ngara akiongea na waandishi wa habari ambapo pamoja na mambo mengine Seikali ya kijiji hicho imekanusha taarifa zilizotolewa na baadhi ya Wananchi kupitia baadhi ya vyombo vya habari  kuwa kuna mauaji ya watu wawili yaliyotokea Kijiji  humo.



Baadhi ya wananchi waliokwenda kuionesha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Ngara eneo la tukio  katika kitongoji cha Ngoma kijiji cha Kasulo.


Baadhi ya wananchi waliokwenda kuionesha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Ngara eneo la tukio  wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Ngara mkoani Kagera Bw. Costantine Kanyasu ambaye aliwataka wananchi wa kijiji  hicho kuacha kijichukulia sheria mkononi na kusababisha maafa katika kijiji chao.



Mwenye gambuti ni Mkuu wa wilaya ya Ngara mkoani Kagera Bw. Costantine Kanyasu akiwa porini  na kamati ya ulinzi na usalama kuangalia sehemu yalikofanyikia mauaji eneo la Ngoma kijiji cha Kasulo wilayani Ngara huku pembeni yake Mwenye suti na notebook ni Mwenyekiti wa kijiji cha Kasulo.

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Ngara ikijianda kuondoka eneo la tukio.
Seikali ya kijiji cha Kasulo wilayani  Ngara mkoani Kagera imekanusha taarifa zilizotolewa na baadhi ya Wananchi kupitia baadhi ya vyombo vya habari  kuwa kuna mauaji ya watu wawili yaliyotokea Kijiji  humo. 

Mwenyekiti wa Kijiji cha Kasulo wilayani Ngara Bw.Yusufu Katula alisema hayo jana(Septemba 26,2013) wakati akiongea na Wananchi wa kitongoji cha Ngoma kilichomo kijijini humo  alipoambatana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Ngara.

Bw.Katula alisema mauaji yaliyofanyika  kijiji humo yaliandaliwa na  waharifu wanaojiita wanaharakati ambapo  wananchi na viongozi kwa kushirikiana na vyombo vya dola wanawasaka ili kuwafikisha kwenye mkondo wa sheria.

Alisema mhamasishaji wa mauaji ambaye alitoroka Bahati Gervas ndiye kichochezi akitafuta umaarufu wa kuwaondoa wahamiaji wenye mifugo eneo la Ngoma licha ya kutokuwa na mchango wa maendeleo kijijini humo.

Mauaji hayo hayahusiani na mmoja wa wafugaji  Athumani Makoye kwani huyo ni mwananchi halali  na mpenda maendeleo maana ametumia fedha nyingi kujenga shule ya kitongoji hiki”…Alisema Katula.

Mauaji hayo yaliyofanyika Septemba 19 ,Mwaka huu yalihusisha kukatwa katwa kwa ng’ombe 15 wenye thamani ya Shilingi Milioni 8.4 mali ya raia wa Rwanda kwa kile kilichoelezwa awali kuwa ni vurugu baina ya wakulima na wafugaji.

Hata hivyo Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Ngara Bw.Costantine Kanyasu aliwataka wananchi wa kijiji  hicho kuacha kijichukulia sheria mkononi na kusababisha maafa katika kijiji chao.

Bw.Kanyasu alisema serikali kwa kushirikiana na wananchi wazalendo tayari wameanza kuwakamata waliohamasisha mauaji  na kwamba hata waliokimbia na kutoroka watawasakwa ili wafikishwe  Mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Habari/Picha Na:-Shaaban Ndyamukama.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad