Gari la wagonjwa (Ambulance) lakamatwa na Jeshi la Polisi likitumika kuiba Mafuta katika Mgodi wa Dhahabu wa Geita( GGM ) huku watuhumiwa 9 wakifikishwa Mahakamani kwa Wizi huo. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, September 27, 2013

Gari la wagonjwa (Ambulance) lakamatwa na Jeshi la Polisi likitumika kuiba Mafuta katika Mgodi wa Dhahabu wa Geita( GGM ) huku watuhumiwa 9 wakifikishwa Mahakamani kwa Wizi huo.

Muonekano wa gari aina ya Land Crusser yenye namba za usajili T 671 AKW ,Mali ya Halmashauri ya wilaya ya Geita  nakuingia mgodini nakuiba mafuta aina ya Diesel lita 630 zenye thamani ya Shilingi 1,386,000/= mali ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM)..
Habari/Picha Na:-Denice Stephano. 
 


Mapipa ya mafuta aina ya Diesel lita 630, mali ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) yakiwa yameibiwa na kupakiwa ndani ya gari aina ya Land Crusser yenye namba za usajili T 671 AKW ,Mali ya Halmashauri ya wilaya ya Geita.  











Gari la wagonjwa (Ambulance) aina ya Land Crusser yenye namba za usajili T 671 AKW ,Mali ya Halmashauri ya wilaya ya Geita likiwa limekamatwa na Jeshi la Polisi Mkoani Geita  kwa tuhuma ya wizi wa mafuta katika mgodi wa Dhahabu( GEITA GOLD MINE ).
Watuhumiwa tisa wa kesi ya wizi wa mafuta katika mgodi wa Dhahabu( GEITA GOLD MINE ) kwa kutumia gari la wagonjwa (Ambulance) wamefikishwa katika Mahakamani ya wilaya ya Geita na kusomewa mashitaka matatu yanayowakabili.

Mwendesha mashitaka wa polisi Inspekta Abiner ameiambia mahakama  kuwa mnamo 05/09/2013 saa 7:30 usiku uko eneo la Geita Power ndani ya mgodi wa Geita Gold Mine watuhumiwa waliiba mafuta lita 630 ya dizeli, kula njama za kuiba mafuta hayo ,kuaribu mali ambayo ni gari la kubeba wagojwa katika kituo cha Afya cha Nzera kwakuling’oa viti.

Mwendesha mashitaka amedai kuwa mtuhumiwa wa kwanza Hamudi Biemo (28) Dereva wa gari hiyo anatuhumiwa kwa makosa matatu likiwemo la kula njama na kung’oa viti vya gari hilo kwa lengo la kubeba mafuta hayo.

Mwendesha mashitaka huyo ameendelea kuiambia mahakama kuwa watuhumiwa 8 wanakabiliwa na makosa 2 ,Wizi wa mafuta na kula njama ya kuiba mafuta hayo.

Abiner ameongeza kuwa washitakiwa hao walitumia gari aina ya Land Crusser yenye namba za usajili T 671 AKW ,Mali ya Halmashauri ya wilaya ya Geita  nakuingia mgodini nakuiba mafuta aina ya Diesel lita 630 zenye thamani ya Shilingi 1,386,000/= mali ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) . 

Waliofikishwa mahakamani ni Hamudi Biembo dereva wa gari la wagonjwa ,Malemo Paul (31)  mkazi wa mtaa wa  Mseto Geita,Selemani Magoso (31 )ambaye ni dereva pikipiki mkazi wa mtaa wa Shilabela Geita, Julias Boazi (28) mkazi wa Msalala road Geita ).

Wengine ni Rashid Hussen (27) Mlizi wa mgodi, Ismail Zuber (26)mlinzi wa Kampuni ya G4S ,Christoper Kombo Operator wa GGM,Joseph Chiristopher (27) Operator wa GGM.


Aidha Wasitakiwa wote (9) wako nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti na kesi yao bado  inaendelea kusikilizwa katika Mahakama ya wilaya ya Geita.

Habari/Picha Na:-Denice Stephano.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad