Mwanamke Raia wa Nigeria adakwa na dawa za kulevya Dar es Salaam , akijianda kusafiri nazo hadi Rome Italia kupitia ufaransa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, September 06, 2013

Mwanamke Raia wa Nigeria adakwa na dawa za kulevya Dar es Salaam , akijianda kusafiri nazo hadi Rome Italia kupitia ufaransa.

Anthonia Ojo (25) akitoa madawa ya kulevya katika makopo ya poda na shampoo baada ya kukamatwa akijianda kusafiri nazo hadi Rome Italia kupitia ufaransa.

Mzigo aliodakwa nao Anthonia Ojo huu hapa.…na Hata hivyo kete hizo 99 hazikujulikana ni za aina gani.

Mtuhumiwa mwenyewe huya hapa Bi.Anthonia Ojo (25), raia wa Nigeria akiwa na amekamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam jana, akieleke Roma, Italia kupitia Paris, Ufaransa kwa ndege ya Ethiopian Airways.

Anthonia Ojo (25) akitoa madawa ya kulevya katika makopo ya poda na shampoo baada ya kukamatwa.

Madawa aliyonaswa nayo Ojo baada ya kutolewa kwenye makopo na yatapelekwa kwa ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali ili kubaini aina ya dawa hizo, thamani yake na hatimaye atafikishwa mahakamani.




Madawa aliyonaswa nayo Ojo baada ya kutolewa kwenye makopo.
Credit: Robert Okanda
Mwanamke mmoja Anthonia Ojo (25), raia wa Nigeria akiwa na kete 99 za madawa ya kulevya amekamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam jana(Septemba 04,2013), akieleke Roma, Italia kupitia Paris, Ufaransa kwa ndege ya Ethiopian Airways.

Mwanamke huyo aliingia hapa nchini Agosti 30 akitokea nchini Nigeria na baada ya kuhojiwa alidai kuwa dawa hizo alizinunua maeneo ya Magomeni, jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Viwanja vya Ndege, Renatus Chalya, Ojo anaendelea kubaki chini ya ulinzi wa polisi kwa uchunguzi zaidi, wakati madawa hayo yakipelekwa kwa ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali ili kubaini aina ya dawa hizo, thamani yake na hatimaye atafikishwa mahakamani.

Kete hizo 99 za dawa za kulevya alikuwa amezihifadhi kwenye chupa ya mafuta ya kupaka na nyingine kwenye kopo la poda za watoto.

Amesema kukakamtwa kwa dawa hizo kunafuatia uwanja huo kufungwa mashine za kisasa za kukagulia mizigo ikiwemo dawa za kulevya.

Aidha pia  raia mmoja wa Urusi aitwae Romani Demichenco akitokea Berlin Ujerumani kupitia Doha - Qatar amekamatwa kwenye uwanja wa ndege Dar es salaam akiwa na vivimiminika vinavyoweza kusababisha milipuko ambapo tayari amefikishwa Mahakamani.


Kukamatwa kwa Watuhumiwa hao, kumekuja wiki tatu tangu Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, kutangaza vita dhidi ya watu wanaopitisha dawa za kulevya katika idara na taasisi zilizoko chini ya wizara yake.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad