Meli ya Tanzania yakamatwa na Dawa za Kulevya Nchini Italia huku Watuhumiwa wakiichoma Moto kupoteza Ushahidi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, September 08, 2013

Meli ya Tanzania yakamatwa na Dawa za Kulevya Nchini Italia huku Watuhumiwa wakiichoma Moto kupoteza Ushahidi.

MV Gold Star ikiungua baada ya kuchomwa moto na wasafirishaji wa madawa ya kulevya. -
-WATUHUMIWA WAICHOMA MOTO KUPOTEZA USHAHIDI, WAJITOSA MAJINI
-ILIKUWA NA DAWA ZA KULEVYA ZENYE THAMANI YA BILIONI 126.5
-MZIGO ULIOKUWEMO NI TANI 30 ZILIZOKUWA  ZINAPELEKWA UTURUKI
-9 WAKAMATWA, NI RAIA WA MISRI NA SYRIA:-Source: Daily Mail


Moshi mkubwa ukitoka katika meli hiyo baada ya wahusika kujitosa majini.

MV Gold Star ikipelekwa katika Bandari ya Sicilia.
MELI iliyosajiliwa nchini Tanzania ya MV Gold Star juzi(Septemba 06,2013), Ijumaa imekamatwa nchini Italia ikiwa na dawa za kulevya zenye thamani ya pauni milioni 50 sawa na shilingi bilioni 126. 5.

Watuhumiwa waliokuwa ndani ya meli hiyo waliamua kuichoma moto ili kupoteza ushahidi na kuamua kupiga mbizi majini lakini walitiwa nguvuni na wanausalama wa Italia.

Meli hiyo ya mizigo ilikuwa imepakia tani 30 za madawa na ilikamatwa jirani na Kisiwa cha Sicilia katika Bahari ya Mediterranian nchini Italia wakati ikielekea Uturuki.

Maofisa wa polisi nchini humo wamedai kuwa watuhumiwa tisa waliokamatwa ni raia wa Misri na Syria na watafikishwa mbele ya sheria.


Moto katika meli hiyo umezimwa na tayari imepelekwa katika Bandari ya Sicilia.

Waziri Mkuu Bw. Mizengo Pinda.
Katika Hatua Nyingine, Waziri Mkuu wa Tanzania ,Bw. Mizengo Pinda amesema kumekuwa na changamoto ya uharakishaji wa mashauri ya dawa za kulevya hali inayoifanya Serikali kufikia hatua ya kufikiria kuwa na mahakama maalumu.

Pinda aliyasema hayo bungeni mjini Dodoma, wakati akiahirisha Mkutano wa 12 wa Bunge hadi Oktoba 29 mwaka huu.

Nina imani tukijipanga vizuri inawezekana. Iko hoja kwamba, labda tutafika mahala tufikirie kuwepo na mahakama maalumu ya dawa za kulevya ambayo itakuwa na kazi moja tu ya kusimamia mashauri yanayohusu dawa za kulevya,” alisema.

Alisema pia vita vya dawa za kulevya ni shirikishi kwa kwa mataifa mbalimbali duniani na kwamba jitihada hizo hufanywa kwa mikutano ya pamoja.

Pinda alisema hii itasaidia misako ya pamoja, mafunzo ya pamoja na matumizi ya vifaa mbalimbali kupangwa.

Vilevile, alisema jitihada nyingine ni kuhamasisha kutunga sheria kali zinazofanana ili kutotoa mwanya kwa watuhumiwa kupenya na kufikisha dawa za kulevya kwa watumiaji.

Ni kweli kwamba, vita vya dawa za kulevya haviwezi kukomeshwa na nchi moja, kwa hiyo mapambano dhidi ya wafanyabiashara haramu wa dawa za kulevya yatafanikiwa tu, kwa nchi zote duniani kuungana kudhibiti biashara hii,” alisema.

Aliwataka wananchi wote kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama, kuwafichua na kutoa taarifa za wote wanaojihusisha na biashara hiyo.

Waziri Pinda alisema kati ya mwaka 2010 hadi Julai, 2013, mashauri 368 yanayohusu dawa za kulevya yalipelekwa mahakamani, kati ya hayo, 91 yalimalizika kwa watuhumiwa kufungwa na wengine kutozwa faini.

Kwa sasa kuna takriban mashauri 245 ambayo bado yako mahakamani. Changamoto inayotukabili katika mahakama zetu na Jeshi la Polisi ni kuharakisha mashauri hayo,” alisema.

Pinda alitumia muda huo pia kueleza kwamba anaiombea Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ijazwe hekima na Mwenyezi Mungu, akisema kazi ya utungaji sheria ni ya wabunge wote.

Alisema hayo kutokana na kitendo cha wabunge hao wa upinzani kususia upitishwaji wa muswada wa Katiba Mpya.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad