![]() |
| Mashabiki wa Simba SC kwa raha zao Taifa leo, Dar es Salaam na kuichapa Mtibwa Sugar Bao 2-0. |
![]() |
| Kikosi cha Simba SC kilichoanza leo dhidi ya Mtibwa Sukari. |
![]() |
| Kikosi cha Mtibwa Sukari kilichoanza leo dhidi ya Simba SC. |
![]() |
| Mashabiki wa Mbya City wakishangilia mchezo wa timu yao na Mabingwa Watetezi Yanga Uwanja wa Sokoine Mbeya na kutoka Sare ya Bao 1-1 na Timu ngumu ya Mbeya City |
![]() |
| Kikosi cha Mbeya City kilichoanza leo dhidi ya Yanga SC. |
![]() |
| Kikosi cha Yanga SC kilichoanza leo dhidi ya Mbeya City |
Ligi kuu soka nchini Tanzania (LIGI KUU
VODACOM)Leo (Septemba 14,2013) ilikuwa dimbani na Mabingwa Watetezi Yanga
walikuwa huko Uwanja wa Sokoine Mbeya na kutoka Sare ya Bao 1-1 na Timu ngumu
ya Mbeya City, wenzao Simba walikuwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na
kuichapa Mtibwa Sugar Bao 2-0 na huko Kaitaba Mjini Bukoba Kagera Sugar ilitoka
Sare Bao 1-1 na Azam FC.
Huko Mbeya,
Wenyeji Mbeya City walitangulia kupata Bao katika Dakika ya 49 alilofunga
Bwigane Yeya na Didier Kavumbagu kuisawazishia Yanga katika Dakika ya 71.
Azam Fc nao
waliponea chupuchupu baada ya kutanguliwa na Kagera Sugar kwa Bao la Themi
Felix katika Dakika ya 25 na Khamis Mcha kurudisha katika Dakika ya 55.
Kwenye
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Simba waliipigiga Mtibwa Sugar kwa Bao za Henry
Joseph Dakika ya 67 na Betram Mombeki Dakika ya 89.
Uwanja wa
Kaitaba mjini Bukoba, Themi Felix Buhaja alitangulia kuifungia Kagera Sugar
dakika ya 25 kabla ya Khamis Mcha ‘Vialli’ kuisawazishia Azam FC dakika ya 55.
Katika mechi
nyingine Coastal Union ilitoka sare ya bila kufungana na Tanzania Prisons
Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, Ruvu Shooting iliifunga 1-0 Mgambo Shooting bao
pekee la Elias Maguri dakika ya 53 Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani, Oljoro JKT
ilitoka sare ya 1-1 Rhino Rangers Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha, wenyeji
wakilazimika kusawazisha dakika ya 27 kupitia kwa Amiri Hamad baada ya Saad
Kipanga kutangulia kuwafungia wageni dakika ya tano, wakati Ashanti United
ililala 1-0 mbele ya JKT Ruvu, Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam bao pekee
la Amos Mgisa dakika ya 81.
Matokeo
hayo, yanamaanisha JKT Ruvu inaendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi zake tisa
baada ya kushinda mechi zote tatu, ikifuatiwa na Simba SC katika nafasi ya pili
yenye pointi saba.
Timu nyingi
zimefungana kwa pointi tano katika nafasi ya tatu, zikiwemo Yanga, Azam na
Coastal Union.
RATIBA LIGI KUU VODACOM 2013/2014.
Septemba 18
Tanzania
Prisons v Yanga
Simba v
Mgambo JKT
Kagera Sugar
v JKT Oljoro
Azam FC v
Ashanti United
Coastal
Union v Rhino Rangers
Mtibwa Sugar
v Mbeya City
Ruvu
Shootings v JKT Ruvu











No comments:
Post a Comment