Al shabaab: ''Walivyolipiza kisasi Kisa 'Kenya ilipuuza onyo letu'' - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, September 22, 2013

Al shabaab: ''Walivyolipiza kisasi Kisa 'Kenya ilipuuza onyo letu''

Taharuki ilianza saa saba mchana Jumamosi (Septemba 21,2013) baada ya watu wanaokisiwa kuwa kumi kuvamia duka kubwa la Nakumat ndani ya jengo la kifahari la Westgate :-Washambuliaji wa kundi la kigaidi la Al Shabaab walivamia jengo hilo na kuwapiga risasi kiholela watu waliokuwemo.



Mwili wa mtu aliyeuliwa nje ya soko kuu la Westgate Mall, lenye maduka ya kifahari mjini Nairobi, Kenya unaonekana siku ya jumamosi Sept. 21 2013, ambako kulitokea shambulio la bunduki na mripuko wa grunetti, kwa mujibu wa Jeshi la Polisi nchini humo.


Baadhi ya watu waliofanikiwa kukimbilia usalama wao.

Mtu aliyejeruhiwa akisaidiwa na mtu mwingine kutoka nje ya soko la Westgate Mall, mjini Nairobi, Kenya siku ya jumamosi Sept. 21 2013, baada ya watu wenye silaha kushambulia na polisi kueleza kwamba lilikuwa shambulio la kigaidi.



Watoa huduma ya kwanza wanamsaidia mtu aliyejeruhiwa baada ya shambulio la bunduki katika soko la Westgate shopping centre, mjini Nairobi Septembea 21, 2013.

 
Watu wakikimbia kujificha wakati polisi wanawasaka washambuliaji walovamia kwa bunduki soko la Westgate jijini Nairobi, Septemba 21, 2013.


Baada ya masaa tano ya taharuki ndani ya jengo hilo milio ya risasi ilikuwa inasikika ishara ya makabiliano kati ya polisi na wanamgambo hao.



Polisi wenye silaha wanawasaka washambuliaji wenye silaha ndani ya soko la Westgate mjini Nairobi, Septemba 21, 2013.


Watu wakikimbia kujificha wakati polisi wanawasaka washambuliaji walovamia kwa bunduki soko la Westgate jijini Nairobi, Septemba 21, 2013.




Watu wakikimbia huku wakiinua mikono juu kutoka soko la Westgate Mall mjini  Nairobi Sept. 21, 2013.

Polisi anajaribu kuhakikisha hakuna mshambuliaji katika eneo alofika baada ya shambulio ndani ya soko la Westgate Nairobi Sept. 20, 2013.

Polisi na Wanajeshi wenye silaha wanawasaka washambuliaji wenye silaha ndani ya soko la Westgate mjini Nairobi, Septemba 21, 2013.

Polisi walijificha ili kujikinga kutokana na shambulio la bunduki katika soko la Westgate ambako washambuliaji wenye bunduki walishambulia na kuchukua baadhi ya wateja mateka mjini Nairobi Septemb 21, 2013.
Hali ni tete katika jiji la Nairobi ambapo washambuliaji wenye silaha Jujmamosi mchana walivamia eneo la kifahari la Westgate Mall nje kidogo ya jiji la Nairobi.

Vyombo vya habari vya Kenya vinaripoti kuwa washambuliaji hao waliokuwa waloficha nyuso zao walivamia maduka hayo mwendo wa saa sita mchana kwa saa za Kenya na kuwateka nyara watu kadha.

Wafanyakazi wengi wamenaswa katika mtafaruku huo huku ikiripotiwa kuwa zaidi ya watu 30 wameuawa.

Polisi wa Kenya wamewaambia wananchi wasiende eneo hilo ambapo kikosi maalum cha kijeshi  KDF kimepelekewa kuwasaka na kukabiliana na washambuliaji hao.

Polisi huko Nairobi wanasema Westgate Mall sasa imedhibitiwa na kikosi maalum cha kijeshi na kwamba kinafanya upekuzi mkali.

Kuna ripoti kuwa mshambualiaji mmoja amekamatwa na msako unaendeela kubaini hasa ni nani waliotekeleza mashambulizi hayo na kwa lengo gani.

Afisaa mmoja mkuu wa kundi la kigaidi la Alshabaab, ameifahamisha BBC kuwa kundi hilo ndilo limehusika na shambulizi dhidi ya duka la kifahari la Westage mjini Nairobi Kenya.

Kwa mujibu wa Afisaa huyo mashambulizi hayo yalikuwa ya kulipiza kisasi kwa Kenya kwa kujihusisha na vita vya Somalia ambako wanajeshi wake wanakabiliana na kundi hilo.

Wanajeshi wa Kenya wamekuwa nchini humo tangu mwaka 2011 kama sehemu ya juhudi za muungano wa Afrika kutaka kurejesha uthabiti nchini Somalia.

Afisaa mkuu wa mambo ya ndani Kenya amesema idadi ya waliofariki ni kumi na moja lakini shirika la msalaba mwekundu linasema idadi hiyo imefika watu 30 huku zaidi ya hamsini wakijeruhiwa.

Taarifa kutoka Ikulu ya Rais Kenya zinasema kuwa mshukiwa mmoja aliyekamatwa alifariki kutokana na majeraha yake.

Wanamgambo wa Al Shabaab kupitia kwa mtandao wao wa Twitter , wanasema kuwa Kenya haikuchukulia kwa uzito onyo walilotoa kwa taifa hilo kwa hatua ya kuwapeleka wanajeshi wake nchini humo kupambana dhidi yao.

Kundi hilo limesema limekuwa likitoa onyo mara kwa mara kwa Kenya kuwa ikiwa haitaondoa vikosi vyake nchini Somalia, athari zitakuwa mbaya mno.

Kupitia mtandao wao wa Twitter, Al Shabaab limesema kuwa Kenya ilijidai kutosikia onyo hizo, na kuendelea kuwaua waisilamu wasio na hatia nchini Somalia.

Taarifa hiyo ya Twitter ilisema kuwa Shambulio la Westgate ni tone tu katika bahari ya mfano wa yanayowakumba wasomali nchini Somalia.

Taharuki ilianza hii leo saa saba mchana wakati watu wanaokisiwa kuwa kumi walipovamia jengo la kifahari la Westgate la kuwapiga risasi kiholela wakenya waliokuwa wanaendelea na shughuli zao za kawaida.


Kwa mujibu wa shirika la msalaba mwekundu , takriban watu 30 walifariki kwa kupigwa risasi au kutokana na majeraha yao na wengine wengi wenye majeraha ya risasi kukimbizwa hospitalini kwa matibabu.

Source Na:-BBC/VOA 

1 comment:

Post Bottom Ad