Ushindi wa Chelsea wawafanya wafikishe Pointi 10 sawa na Liverpool lakini wao wako juu kwa ubora wa Magoli lakini huenda Msimo huo ukabadilika Jumapili ambapo Chelsea wanaweza kuporwa uongozi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, September 22, 2013

Ushindi wa Chelsea wawafanya wafikishe Pointi 10 sawa na Liverpool lakini wao wako juu kwa ubora wa Magoli lakini huenda Msimo huo ukabadilika Jumapili ambapo Chelsea wanaweza kuporwa uongozi.

CHELSEA:-Ushindi huo wa 2-0 unamaanisha Fulham inatimiza miaka 34 bila kushinda Stamford Bridge, Chelsea ikizinduka baada ya vipigo vya Everton na FC Basle.
 Mchezaji kiungo John Obi Mikel amefunga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu ya Uingereza na kuiwezesha Chelsea kuibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Fulham Uwanja wa Stamford Bridge, huo ukiwa ushindi wao wa kwanza mwezi huu.

Mabao ya Oscar na Mikel kipindi cha pili yamemaliza ukame wa ushindi ndani ya mechi nne na kuendeleza rekodi ya Jose Mourinho kutofungwa nyumbani katika Ligi Kuu ndani ya mechi 63 na ushndi wa kwanza tangu wafungwe na Aston Villa.

Ushindi huu umewafanya Chelsea wafikishe Pointi 10 sawa na Liverpool lakini wao wako juu kwa ubora wa Magoli lakini huenda Msimo huu ukabadilika hapo kesho baada ya Mechi 4 za Jumapili ambapo Chelsea wanaweza kuporwa uongozi.

John Obi Mikel akifunga bao lake la kwanza Ligi Kuu Uingereza , akicheza Mechi yake ya 185 ya Ligi na leo (September 21,2013) ndio ameona nyavu kwa mara ya kwanza alipofunga Bao la Pili katika Dakika ya 84.

Jose Mourinho akishangilia ushindi wake wa kwanza mwezi huu ambapo Pia ushindi huu umepokewa kwa furaha kwa wadau wa Chelsea baada ya kufungwa mfululizo Mechi mbili zilizopita.

Mwenye timu tabasamu latosha: Roman Abramovich akiwa jukwaani kuangalia ushindi wa timu yake.


Oscar alituliza mchecheto wa Chelsea baada ya Kipa David Stockdale kutema shuti la Samuel Eto'o na yeye kufunga.


Ushindi huu umewafanya Chelsea wafikishe Pointi 10 sawa na Liverpool lakini wao wako juu kwa ubora wa Magoli lakini huenda Msimo huu ukabadilika hapo kesho baada ya Mechi 4 za Jumapili ambapo Chelsea wanaweza kuporwa uongozi.

LIVERPOOL:- Wachezaji wa Liverpool wakiangalia mpira uliopigwa kwa kichwa na Lovren ukitinga nyavuni.
BAO pekee la Dejan Lovren limeipa Southampton ushindi wa 1-0 Uwanja wa Anfield dhidi ya wenyeji Liverpool Jana(Septemba 21,2013).

Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Croatia alifunga bao hilo dakika ya 54 na kumaliza rekodi ya Liverpool kutofungwa ndani ya mechi 12.

Pamoja na hayo The Saints, inabidi wamshukuru refa Neil Swarbrick aliyewanyima Liverpool penalti baada ya beki wao kumuangusha Daniel Sturridge kwenye eneo la hari kipindi cha kwanza.

Dejan Lovren amfunga bao pekee la ushindi dhidi ya Liverpool na hapo akishangilia mbele ya mashabiki wa Southampton.

Daniel Sturridge aisikitika baada ya kupoteza nafasi ya kufunga katika mchezo huo ambao Liverpool wameupoteza kwa kufungwa bao 1-0.




Mshambuliaji Luis Suarez, alikuwepo jukwaani akishuhudia mechi yake hiyo ya mwisho katika adhabu ya kufungiwa mechi 10 na sasa anarejea uwanjani.
 LIGI KUU UINGEREZA MATOKEO.
Jumamosi 21 Septemba,2013.

Hasira: Brendan Rodgers.
Norwich City 0 Aston Villa 1

Liverpool 0 Southampton 1

Newcastle United 2 Hull City 3

West Bromwich Albion 3 Sunderland 0

West Ham United 2 Everton 3

Chelsea 2 Fulham 0

RATIBA
[Saa za Bongo]
Jumapili 22 Septemba,2013.


15:30 Arsenal v Stoke City

15:30 Crystal Palace v Swansea City

18:00 Cardiff City v Tottenham Hotspur


18:00 Manchester City v Manchester United


MSIMAMO-TIMU ZA JUU 2013/2014 :- EPL.

NA
TIMU
P
PTS
1
Chelsea
5
10
2
Liverpool
5
10
3
Arsenal
4
9
4
Tottenham
4
9
5
Everton
5
9
6
Southampton
5
8
7
Man. City
4
7
8
Man. United
4
7
9
Stoke City
4
7
10
Hull City
5
7

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad