Tazama Wilaya ya Ngara ,mkoani Kagera nchini Tanzania kupitia timu ya Walimu FC na Ziara yake ya Kimichezo wilayani Giteranyi,Mkoa wa Muyinga nchini Burundi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, June 17, 2013

Tazama Wilaya ya Ngara ,mkoani Kagera nchini Tanzania kupitia timu ya Walimu FC na Ziara yake ya Kimichezo wilayani Giteranyi,Mkoa wa Muyinga nchini Burundi.


Mchezo wa Wavu ama Volleyball , Ngara Volleyball ikawafunga wenyeji Ingo Nawe Seti 3-0 ,Mchezo ukichezwa katika Uwanja wa Volleyball,Giteranyi nchini Burundi Juni 09,2013.




Mashabiki wa timu ya Ngara Volleyball wakishangilia ushindi wa kisasi dhidi ya Ingo Nawe Volleyball baada ya Ngara Volleyball kuwafunga wenyeji Ingo Nawe Seti 3-0 ,Mchezo ukichezwa katika Uwanja wa Volleyball,Giteranyi.




Mashabiki wakifatilia mchezo wa Wavu ama Volleyball , kati ya Ngara Volleyball na wenyeji Ingo Nawe  ,Mchezo ukichezwa katika Uwanja wa Volleyball,Giteranyi ,japo wenyeji walifungwa seti 3 - 0 lakini ulikuwa mkali na wakusisimua kwa mashabiki wote .


Hiki ni Kikosi cha wachezaji 11 cha Ingo Nawe FC kilichoanza Mchezo wa kirafiki wa Kimataifa uliofanyika Juni 09,2013, katika uwanja wa wilaya ya Giteranyi  na wenyeji-Ingo Nawe  kutoa sare ya bao 2 – 2 na Walimu FC.


Hiki ni Kikosi cha wachezaji 11 cha Walimu FC kilichoanza Mchezo wa kirafiki wa Kimataifa uliofanyika Juni 09,2013, katika uwanja wa wilaya ya Giteranyi  na wenyeji-Ingo Nawe  kutoa sare ya bao 2 – 2 na Walimu FC.


Golikipa wa Timu ya Walimu FC Mwl.Gilman Mtegoa akitazama mpira uliopigwa na wapinzani wao Ingo Nawe FC pembezeno mwa lango lake katika mchezo wa Soka na timu hizo kutoka sare ya bao 2-2  ,Mchezo ukichezwa katika Uwanja wa soka ,Giteranyi.


Timu ya Walimu FC ilijikaza kiume na kulazimisha dakika 90 za mchezo wake na wanyeji timu ya Ingo Nawe  toka wilayani Giteranyi nchini Burudni kumalizika kwa matokeo ya sare ya kufungana bao 2-2.




Mchezo huo wa kirafiki wa Kimataifa uliofanyika Juni 09,2013, katika uwanja wa wilaya ya Giteranyi  na wenyeji-Ingo Nawe  kutumia vema uwenyeji wao kuandika mabao 2 kipindi cha kwanza cha mchezo huo kupitia kwa wachezaji wao Samweli Eton a Glasia Ntukamazina.




Kipindi cha pili kilipoanza ,Walimu FC walibadilika na Kulinda heshima ya wilaya ya Ngara kwa kupigana kiume kukomboa magoli hayo mawili yaliyofungwa na wachezaji wao Mwl.Festo Chiwanga na Sevelin John.




Kocha wa Ingo Nawe Nibaza Antoni licha ya Kufurahia mchezo huo wa kirafiki katika kuboresha mahusiano mema ila uwanja kutokuwa na kiwango bora cha kuchezewa ndicho kiliwaponza na kuruhusu kutoka sare.




Kwa upande wake Faustin Malulu katibu Mkuu wa Klabu ya Walimu FC alisemaje kuwa  Matokeo hayo ya sare  yanatoa picha nzuri kwa Klabu yake hasa hivi sasa ikiwa katika mkakati wa kujiboresha na kuomba Wadau kuisaidia kwa hali na mali ili ifikie malengo ya kuwa tibu bora.




Katika Matokeo ya  Mchezo wa Wavu ama Volleyball , Ngara Volleyball ikawafunga wenyeji Ingo Nawe Seti 3-0 na  kumfanya Kocha wa timu ya mchezo huo ya Ingo Nawe Joni Belikimas Mbogambi kukubali kipigo hicho bila kupepesa maneno kuwa Ngara walijiandaa vya kutosha na kumudu kila idara  zaidi yao.




Katika mchezo wa Mpira wa Kikapu ama Basketball licha ya kukumbwa na utata wa maamuzi kutoka kwa waamuzi wa mchezo huo Baby wa Ngara na Kleva wa Giteranyi,Wenyeji Ingo Nawe wakatalwa na kuwafunga Ngara Vikapu 39 – 31.



Katika hatua Nyingine mkuu wa mkoa wa Muyinga nchini Burundi Idefonsi Ntahunkunda amesema kuwa ziara ya kimichezo waliyoifanya wilaya ya Ngara kupitia timu ya Walimu FC  imehamasisha ujirani mwema,amani na ushirikiano katika wilaya yao ya Giteranyi na kwamba Serikali ya Mkoa wa Muyinga itajipanga kuwasiliana na Serikali ya mkoa wa Kagera nchini Tanzania kuona namna nzuri ya kuboresha ujirani mwema kupitia Michezo.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad