Ivory Coast waichapa Tanzania bao 4-2 ikiwa ni mchezo wa kusaka Timu 5 zitakazocheza Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwaka 2014. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, June 16, 2013

Ivory Coast waichapa Tanzania bao 4-2 ikiwa ni mchezo wa kusaka Timu 5 zitakazocheza Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwaka 2014.


Mechi kadhaa za Makundi Barani Afrika kusaka Timu 5 zitakazocheza Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwaka 2014 na Katika KUNDI C, ambalo leo(Juni 16,2013) , Tanzania imeikaribisha Ivory Coast Jijini Dar es Salaam, Ivory Coast ndio Vinara wakiwa na Pointi 13 baada ya Kuifunga Taifa Starz bao 4 – 2,kwa magoli ya Traore mawili,Yaya Toure na Wilfreid, Morocco Pointi  8, Tanzania Pointi  6 na Gambia  Pointi  1.


Wachezaji wa Ivory Coast wakishangilia Ushindi wao wa bao 4-2 dhidi ya Tanzania katika  mchezo wao uwanja wa Taifa –Tanzania  ikiwa ni mchezo wa leo(Juni 16,2013) kusaka Timu 5 zitakazocheza Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwaka 2014.


Mashabiki wa Taifa Starz wakishuhudia timu yao ikipoteza  Pointi 3 muhimu mbele ya, Ivory Coast ndio Vinara wakiwa na Pointi 13 baada ya Kuifunga Taifa Starz bao 4 – 2,kwa magoli ya Traore mawili,Yaya Toure na Wilfreid, Morocco Pointi  8, Tanzania Pointi  6 na Gambia  Pointi  1.


Morocco Jana(Juni 15,2013)  waliipikua Tanzania Nafasi ya Pili ya KUNDI C baada ya kuichapa Timu ya mkiani Gambia kwa Bao 2-0 katika Mechi iliyochezwa huko Marrakech.


Bao za Morocco zilifungwa na Barrada na Younes Belhanda.



Katika KUNDI C, ambalo leo(Juni 16,2013) , Tanzania imeikaribisha Ivory Coast Jijini Dar es Salaam, Ivory Coast ndio Vinara wakiwa na Pointi 13 baada ya Kuifunga Taifa Starz bao 4 – 2,kwa magoli ya Traore mawili,Yaya Toure na Wilfreid, Morocco Pointi  8, Tanzania Pointi  6 na Gambia  Pointi  1.



Ivory Coast imefanikiwa kusonga hatua ya pili na ya mwisho katika kuwanai tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia na Kwa ushindi huo, Ivory Coast imetimiza pointi 13 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine yoyote katika kundi hilo na sasa itasubiri kucheza na mmoja wa washindi wengine wa makundi mengine tisa ili kuwania kwenda Brazil mwakani.


Straika wa Uganda, Emmanel Okwi Jana aliifungia Uganda Bao muhimu katika Mechi yao ya KUNDI J la kuwania kwenda Brazil Mwaka 2014 kucheza Fainali za Kombe la Dunia walipoifunga Angola Bao 2-1 na kutwaa uongozi wa Kundi hilo.



Katika Mechi hiyo, Angola walitangulia kufunga kupitia Job lakini Uganda walipiga Bao 2 Wafungaji wakiwa Emmanuel Okw na Tonny Mawejje.



Ushindi huo umewafanya Uganda wawe juu ya Senegal kwa Pointi 2 na leo huko Monrovia Lineria itacheza na Senegal.



Kwenye KUNDI E, waliokuwa Vinara, Congo wakiwa Nyumbani Pointe Noire, walijikuta wakipoteza uongozi huo kwa kuchapwa Bao 1-0 na Burkina Faso kwa Bao la Aristide Bance na sasa Burkina Faso wako kileleni Pointi 2 mbele ya Congo.




Morocco 2 Gambia 0.
Burkina Faso ndio walimaliza wa pili nyuma ya Mabingwa Nigeria kwenye AFCON 2013.



Katika Mechi nyingine ya KUNDI E, Hetitriki ya Pierre-Emerick Aubameyang iliwapa ushindi wa Bao 4-1 Gabon dhidi ya Niger na kuwa Pointi 2 nyuma ya Vinara Burkina Faso.



Wakiwa kwao, Zambia jana walibanwa na kutoka Sare ya Bao 1-1 na Sudan ambayo haina matumaini ya kusonga mbele.



Matokeo hayo yamewafanya leo Ghana, ambao wako Ugenini kucheza na Lesotho, kuwa na nafasi murua kutwaa uongozi wa KUNDI D ikiwa watashinda na kujiweka kwenye hali nzuri kucheza na Zambia huko Accra katika Mechi yao ya mwisho ya Kundi.


RATIBA/MATOKEO:




[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya kwanza]



Ijumaa Juni 14,2013.




Libya 2 Togo 0



Jumamosi Juni 15,2013.




Botswana 3 Central African Republic 2



Zambia 1 Sudan 1



Uganda 2 Angola 1



Congo 0 Burkina Faso 1



Gabon 4 Niger 1



Cape Verde 1 Sierra Leone 0



Morocco 2 Gambia 0



Jumapili Juni 16,2013.





16:00 Lesotho v Ghana [0-7]



16:00 Mozambique v Egypt [0-2]



16:00 Ethiopia v South Africa [1-1]



16:30 Rwanda v Algeria [0-4]



17:30 Congo, DR v Cameroon



19:00 Liberia v Senegal [1-3]



20:00 Guinea v Zimbabwe [1-0]



20:00 Equatorial Guinea v Tunisia [1-3]



21:00 Mali v Benin [0-1]



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad