Mungu amrehemu,Marehemu Albert Mangweha azikwa kishujaa kwenye makaburi ya Kihonda mkoani Morogoro. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Thursday, June 06, 2013

demo-image

Mungu amrehemu,Marehemu Albert Mangweha azikwa kishujaa kwenye makaburi ya Kihonda mkoani Morogoro.

.com/simgad/
bb21b674cea911e2918122000a9f4d8a_7

Hapa ndipo Mwili wa Marehemu Albert Mangwea ulipopumzishwa leo (Juni 06,2013) Mkoani Morogoro.



Baada ya siku kadhaa zilizokuwa na kila aina ya harakati, ugumu na majonzi makubwa, Albert Mangweha aka Ngwair hatimaye leo amezikwa kwenye makaburi ya Kihonda mkoani Morogoro ambako ni nyumbani kwao.



Kabla ya kuzikwa, wananchi wa Mkoa wa  Morogoro walipata fursa ya kuuaga mwili wake kwenye uwanja wa Jamhuri.



Umati mkubwa wa wananchi ulijitokeza kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Ngwair aliyefariki nchini Afrika Kusini, wiki iliyopita.



 Wasanii wengi kutoka Dar es Salaam nao wamehudhuria mazishi hayo.
ee9d94facea411e2a9ea22000ae81462_7

f18745b2cea411e2aa3022000a9e2931_7


Marehemu Albert Mangweha azikwa kishujaa sana ni umati usioelezeka mungu akulaze mahali pema peponi,” ameandika Izzo B kwenye Instagram.




Naye Lady Jaydee kupitia Twitter ameandika: Mpaka hapa tulipomsindikiza panatosha. Mungu amrehemu, kazi tumeimaliza. Life goes on.”
e1147594cea211e2a86422000a1f9839_7

75e8603ecea511e29ecd22000aaa08de_7
4406673ccea511e2850422000a1f9a85_7

e1147594cea211e2a86422000a1f9839_7

Marehemu Ngwear alizaliwa Novemba 16 mwaka 1982 huko Mbeya, huku asili yake ikiwa ni Mkoa wa Ruvuma akiwa mtoto wa mwisho katika familia yao.




Ngwea alitambulika katika sanaa ya muziki wa Bongo Fleva, hasa baada ya wimbo wake wa Ghetto Langu kupokewa kwa shangwe na mashabiki wake, akitoa nyimbo nyingine nzuri, kama vile Mikasi, Mimi, She Got a Gwan, Speed 120, CNN na nyinginezo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *