UMITASHUMTA Ngazi ya Mkoa wa Kagera,Wilaya ya Ngara imeanza Vyema kwa Kupata Ushindi katika mbio 100 na 200. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Thursday, June 06, 2013

demo-image

UMITASHUMTA Ngazi ya Mkoa wa Kagera,Wilaya ya Ngara imeanza Vyema kwa Kupata Ushindi katika mbio 100 na 200.

.com/simgad/
2013-05-31+15.56.34

Kabla ya Wilaya ya Ngara Mkoani Kagera kupata Kikosi cha wanamichezo  mbalimbali wapatao 78 kuiwakilisha Wilaya hiyo Katika Mashindano ya michezo mbalimbali kwa Shule za Msingi nchini UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa wa Kagera,Kiliendesha Mashindano hayo Ngazi ya Shule,Kata na Tarafa ambapo Ushindi wa Jumla Kiwilaya Ulikwenda kwa Tarafa ya Nyamiaga.



Katika Matokeo ya Jana(Juni05,2013) kwenye UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa wa Kagera,Wilaya ya Ngara imeanza Vyema kwa Kupata Ushindi katika mbio 100 na 200 wakiibuka washindi wa pili Kimkoa Wavulana na Washichana,Mpira wa miguu Wakiifunga bao 4-0 wilaya ya Karagwe,Netballa 10 -7 Bukoba Vijijini,Volleyball Ngara set 2-1 Karagwe,Handball-Ngara 9-10 Bukoba Vijijini huku wakicheza vizuri Soka ,Volleyball na Netball.


2013-05-31+15.55.46


Ni mchezo wa Soka kati ya Tarafa ya Nyamiaga na Murusagamba katika uwanja wa shule ya sekondari Kabanga wilayani Ngara ,ambapo Tarafa ya Nyamiaga waliwafunga Murusagamba bao 1-0 na Kuwa Mabingwa katika mchezo huo wakifatiwa na Murusagamba ,Tarafa ya Kanazi na Rulenge.

2013-05-31+15.57.10

2013-05-31+16.11.50

Katika Matokeo ya Jana(Juni05,2013) kwenye UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa wa Kagera,Wilaya ya Ngara imeanza Vyema kwa Kupata Ushindi katika mbio 100 na 200 wakiibuka washindi wa pili Kimkoa Wavulana na Washichana,Mpira wa miguu Wakiifunga bao 4-0 wilaya ya Karagwe,Netballa 10 -7 Bukoba Vijijini,Volleyball Ngara set 2-1 Karagwe,Handball-Ngara 9-10 Bukoba Vijijini huku wakicheza vizuri Soka ,Volleyball na Netball.

2013-05-31+16.34.49

2013-05-31+18.09.44

2013-05-31+16.35.33

Mwalimu wa Michezo toka Tarafa ya Nyamiaga Adof  Gisuka  na Mwenzie  wakifatilia Michezo  wa Soka kati ya Tarafa ya Nyamiaga na Murusagamba kwenye mbalimbali ya UMITASHUMTA ngazi ya Wilaya ya Ngara Mkoani Kagera.

2013-05-31+15.07.27

Said Salum Afisa Michezo wilaya ya Ngara anayeandika ,Afisa Taaluma wilaya Osward Rujuba wakifatilia Michezo mbalimbali ya UMITASHUMTA ngazi ya Wilaya ya Ngara Mkoani Kagera.

2013-05-31+18.10.45

MC ambaye ni Kaimu Afisa Michezo wilaya ya Ngara -Bakari akiendesha zoezi la Kuwataja washindi wa Jumla Kiwilaya baada ya kukamilika kwa  Michezo mbalimbali ya UMITASHUMTA ngazi ya Wilaya ya Ngara Mkoani Kagera.

2013-05-31+18.14.12

Vikombe na Vyeti vilitolewa kama ni zawadi kwa washindi wa Jumla Kiwilaya kwenye  Michezo hiyo  ya UMITASHUMTA ngazi ya Wilaya ya Ngara Mkoani Kagera.


2013-05-31+18.37.25

Toka kushoto ni Afisa Michezo wilaya ya Ngara Said Salum,Afisa Elimu wilaya Saimon Mumbee na Diwani wa Kata ya Kabanga Said Sud wakitoa zawadi ya Vikombe na Vyeti kwa washindi katika mashindano ya  UMITASHUMTA ngazi ya Wilaya ya Ngara kwenye Viwanja Vya Shule ya Sekondari Kabanga.

2013-05-31+19.02.43

Mratibu Elimu Taraafa ya Nyamiaga Sospiter Mtegoa  akionyesha zawadi walizopata ya Vikombe Viwili na Vyeti  na kuwafanya Kuibuka washindi wa Jumla Kiwilaya katika mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya Wilaya ya Ngara  .

2013-05-31+15.08.42

2013-05-31+15.09.27

Mwenye suti ya Kaki ni Diwani wa kata ya Kabanga na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi(CCM) Wilaya ya Ngara,Said Sudi akifatilia mchakato wa kupata timu ya Halmashauri ya wilaya ya Ngara,iliyokwenda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa wa Kagera.

2013-05-31+18.48.46

Hiki ndicho Kikosi cha wanamichezo  mbalimbali wapatao 78 kutoka Halimashauri ya wilaya ya Ngara mkoani Kagera Kiko huko wilayani Muleba mkoani Kagera ,kupambana kwa siku 3 katika Mashindano ya michezo mbalimbali kwa Shule za Msingi nchini UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa wa Kagera.
2013-05-31+16.12.10

Huu ni muonekano wa Viwanja vya Michezo mbalimbali Vilivyopo katika shule ya Sekondari Kabanga wilayani Ngara Mkoa wa Kagera.


Kikosi cha wanamichezo  mbalimbali wapatao 78 kutoka Halimashauri ya wilaya ya Ngara mkoani Kagera Kiko huko wilayani Muleba mkoani Kagera ,kupambana kwa siku 3 katika Mashindano ya michezo mbalimbali kwa Shule za Msingi nchini UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa wa Kagera ,mashindano yaliyoanza Juni 05 hadi Juni 08 ,2013 katika Viwanja vya Michezo vya Chuo cha Ualimu Katoke.



Akikiaga kikosi hicho ,mkuu wa wilaya ya Ngara na mwenyekiti wa Michezo Costantine Kanyasu licha ya kuwataka Vijana hao kudumisha nidhamu ya kiuchezaji wawapo uwanjani pia wamewataka kuweka nia ya ushindi na mazoezi katika umri wao mdogo michezoni  ili kukuza vipaji vyao pamoja na kupata mafanikio.



Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara Joni Shimilimana  amewataka kupigana kwa dhati katika mashindano hayo ili kuleta ushindi .



Nae mdau wa michezo hapa wilayani na Mjumbe wa NEC taifa CCM Issa Husein Samma amesema michezo ni ajira hivyo kuwataka vijana hao kujibidiisha na kujituma ili kupata matunda mazuri kupitia Michezo.


Mashindano  hayo ya michezo mbalimbali kwa shule za msingi UMITASHUMTA ngazi ya mkoa wa Kagera yanashirikisha jumla ya wanafunzi zaidi ya 500 kutoka wilaya saba za Mkoa wa Kagera ambazo ni pamoja na  Ngara,Bukoba,Manispaa,Karagwe,Biharamulo,Misenyi na Muleba .



Kwa Mujibu wa Afisa Michezo mkoa wa Kagera Kefa Eliasi amesema  mashindano hayo ya UMITASHUMTA Ngazi ya mkoa wa Kagera kwa mwaka huu yanashindanishwa katika Michezo ya Mpira wa Miguu(Soka),Mpira wa Pete(Netball),Mpira wa Wavu (VolleyBall),Mpira wa Kikapu(Basketball),Riadha(mita 100,200,400,800,1500 na 3000),Handball,Mitupo  na Miluko.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *