Brazil na Italy zatinga Nusu Fainali ya Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara, Mexico na Japan kutupwa nje ya Mashindano toka Kundi A. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, June 20, 2013

Brazil na Italy zatinga Nusu Fainali ya Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara, Mexico na Japan kutupwa nje ya Mashindano toka Kundi A.


Neyman akishangilia baada ya kufunga bao tamu ndani ya dakika 10 za kwanza kabla ya kumtengenezea nafasi ya kufunga bao la pili Jo kwa kuilaza Mexico mabao 2-0 bila ubishi na sasa inatimiza ponti sita na kuzidi kujiimarisha kileleni mwa Kundi A la Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara ilichezwa kati ya Italy na Japan na kushuhudia piga nikupige iliyomalizika kwa ushindi wa Italy wa Bao 4-3.


Wachezaji wa Brazil wakishangilia ushindi wao kwa kuilaza Mexico mabao 2-0 bila ubishi na sasa inatimiza ponti sita na kuzidi kujiimarisha kileleni mwa Kundi A.





Nayman akimtoka beki wa Mexico katika mchezo wa Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara na Brazil kushinda bao 2-0.


Timu ya taifa ya Brazil imeshinda mechi yake ya pili ya Kombe la Mabara, huku kijana mdogo mwenye kipaji cha ajabu, Neymar akifunga bao tamu ndani ya dakika 10 za kwanza kabla ya kumtengenezea nafasi ya kufunga bao la pili Jo.




Brazil imeilaza Mexico mabao 2-0 bila ubishi na sasa inatimiza ponti sita na kuzidi kujiimarisha kileleni mwa Kundi A.




Daniel Alves alipinda krosi kutoka kulia na nyota mpya wa Barcelona, Neymar akaitokea wa kwanza mbele ya beki wa Mexico, kabla ya kuhadaa na kumtungua kipa Jose Corona dakika ya tisa na dakika ya 90 akampa pande Jo kufunga la pili.




Katika  Mechi ya pili ya Kundi A la Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara ilichezwa kati ya Italy na Japan na kushuhudia piga nikupige iliyomalizika kwa ushindi wa Italy wa Bao 4-3.



Matokeo hayo yalihakikisha Wenyeji Brazil na Italy kuingia Nusu Fainali na Mexico na Japan kutupwa nje ya Mashindano toka Kundi A.




Alhamisi (Juni 20,2013) Usiku, Kundi B watacheza Mechi zao za pili na Mabingwa wa Dunia Spain watacheza na Tahiti na kufuatia Mechi ya Mabingwa wa Afrika Nigeria dhidi ya Uruguay.




Spain na Nigeria zilishinda Mechi zao za kwanza kwa Spain 2 Uruguay 1 na Tahiti 1 Nigeria 6.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad