Bila shaka Kocha Mourinho yu tayari kujipanga kuipa Chelsea taji la kwanza la Ligi Kuu ya England msimu ujao tangu mwaka 2010. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Tuesday, June 04, 2013

demo-image

Bila shaka Kocha Mourinho yu tayari kujipanga kuipa Chelsea taji la kwanza la Ligi Kuu ya England msimu ujao tangu mwaka 2010.

.com/simgad/


article-2335102-1A20B7D9000005DC-898_634x394
Jose Mourinho.
Klabu  ya Chelsea imemteua tena Jose Mourinho kuwa meneja wa klabu hiyo kwa Mkataba wa miaka minne na atarejea katika klabu ambayo alishinda mataji mawili ya Ligi Kuu ya England, Kombe la FA na mawili ya Kombe la Ligi  kati ya mwaka 2004 na 2007.




Mourinho ambaye ni raia wa Ureno atachukua nafasi ya Kocha Rafael Banitez aliyejiunga na Klabu ya Napoli ya Italia  baada ya kuinoa klabu hiyo kwa miezi sita.




 Hii ni mara ya pili kwa Mourinho kurejea Stamford Brigde kama kocha baada ya kuondoka miaka sita iliyopita. 




Mourinho ndiye alikuwa chaguo la kwanza la mmiliki wa klabu hiyo Roman Abramovich baada ya kuinunua klabu hiyo mwaka 2003 na ndiye kocha pekee kati ya tisa waliopita klabuni hapo kuanzia kipindi hicho aliyeipa mafanikio zaidi.




Mourinho ametua na benchi lake la ufundi linaloundwa na Rui Faria, Silvino Louro na Jose Morais aliokuwa nao Real, ambao watafanya kazi pamoja na benchi la ufundi la sasa la timu ya kwanza, Steve Holland, Christophe Lollichon na Chris Jones,"ilisema taarifa ya Chelsea.




Bila shaka Kocha  Mourinho yu tayari kujipanga kuipa Chelsea taji la kwanza la Ligi Kuu ya England msimu ujao tangu mwaka 2010.




Taarifa katika tovuti ya klabu hiyo imesema: "Klabu ya soka ya Chelsea inayo furaha kutangaza kuteuliwa kwa Jose Mourinho kama Kocha Mkuu wa kikosi cha kwanza.


article-2335102-1A20B4D4000005DC-486_634x375

article-2335102-1A20B692000005DC-224_634x513


Jose Mourinho akiwa ameshika jezi ya Chelsea baada ya kuthibitishwa kocha mpya wa Chelsea.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *