Safari ya Rais Obama itaanza Juni 26 mpaka Julai 3 na inalenga kudhihirisha mahusiano ya karibu kati ya Marekani na nchi za Afrika, kusini mwa jangwa la Sahara. |
Tayari White House inasema Rais wa Marekani Barack Obama
atakwenda Afrika mwishoni mwa mwezi wa
sita ambapo atazuru nchi tatu.
Katika
taarifa , White House
ilisema rais Obama na mke wake Michelle watakwenda Senegal, Afrika Kusini na Tanzania mwishoni mwa Juni
na mapema mwezi Julai.
Utawala wa Rais Obama unasema Rais huyu wa Marekani
atakutana na maafisa wa serikali, viongozi wa kibiashara, asasi za kiraia na
makundi ya vijana.
Safari ya Rais Obama itaanza Juni 26 mpaka Julai 3 na inalenga kudhihirisha mahusiano ya
karibu kati ya Marekani na nchi za Afrika, kusini mwa jangwa la Sahara.
Rais Obama
ambaye baba yake alizaliwa Kenya, alizuru Afrika mara moja
katika muhula wake wa kwanza, alipotembelelea Ghana mwaka 2009.
Mkewe
Michelle Obama pia amesafiri kwenda Afrika Kusini na Bostwana.
No comments:
Post a Comment